Posts

Showing posts from May, 2025

241. Sisi Tukusanyikapo Hapa

Sisi tukusanyikao hapa  twapeana mikono  tuyakumbuke mateso yako,  tusijitenge nawe. Nayo kazi hii ya roho zetu  kama inakupendeza Bwana,  utujibu:  Amen, tutulie mioyo! 

242. Tumsifu Mungu Bwana

1. Tumsifuni Mungu     Bwana Mtakatifu     anatawala vizuri popote,     asiyekubali wabaya watutese,    tumsifu Mungu wetu,     hakutusahau. 2. Tulipoumia alituokoa,     atusaidia tulio wake.    Nasi twawashinda     maadui popote,    sababu Bwana wetu     anatuongoza. 3. Twamsifu Mwenyezi     aliye mbinguni.     Twamwomba:    “Uzidi kutubariki,     mwovu asipate      kutudhuru kwa hila,”     twasifu Jina lako,      Mwokozi wetu mkuu.

243. Wazima Wote Wamsifu

Wazima wote wamsifu Bwana,  Wazima wote wamsifu Bwana!  Msifu Bwana, Msifu Bwana.  Nyumbani mwake tumshangilie  nguvu zake za juu tuzisifu!  Wazima wote, msifu Bwana,  wazima wote, wazima wote,  Wamsifu Bwana! Wamsifu Bwana! Kwa filimbi na baragumu  na vinubi hata zeze na ngoma  wamsifu Bwana, wamsifu Bwana.  Wazima wote, wamsifu Bwana  baragumu na filimbi   wamsifu Bwana,  Ee, Bwana wa Majeshi. Haleluya. 

244. Kristo Usituondoke

1.  Kristo usituondoke      sababu mchana waisha,     mwanga wa Neno la Mungu     usiuzimishe kwetu! 2.  Nyakati hizi za mwisho      tusaidie kushika      Neno la huruma yako      nalo fumbo takatifu.  3.  Kundi lako ulilinde      ulikusanye mwenyewe,      libariki Neno lako,       litangaziwe popote! 4.  Mambo na mashauri yote      si yetu ila ni yako,     kwa hiyo wasimamishe      wanaokutegemea. 5.  Neno lako ngome kubwa,     hata boma la makundi;      kwa Neno lako tulishe      tusitafute mengine!

245. Huruma Zako Ni Nyingi

1. Huruma zako ni nyingi     Yesu siku kwa siku,     mapenzi yako yapita     kiasi cha maneno! 2. Watupenda na kutoa     damuyo msalabani,    watakatifu wapenda     kumwona Mungu wao. 3. Watupenda tangu mwanzo,     ni mwanzo wa furaha.     Mwisho wa kutegemea    ni kukuona wewe. 4. Tujue, Bwana, Mkombozi,    utupendavyo sasa     mpaka tutakapokufa,     tutakuona wewe.

246. Wenzetu Leo Hii Twawaaga

1. K:  Wenzetu leo hii         twawaaga kweli    W:  Muende salama.     K:  Njiani muwe na         safari ya heri;    W:  Mlindwe na Bwana.      K:  Kweli     W:  Mfike salama.      K:  Nyumbani     W:  Muone jamaa. 2. K:  Tunayo huzuni,         furaha, sababu     W:  Ninyi mwatutoka.      K:  Lakini tunayo         imani kwa Mungu     W:  Kwamba tu pamoja,     K:  Katika    W:  Sala za imani.     K:  Twaona    W:  Umoja wa kweli. 3. K:  Twamsifu Bwana         kwa kazi yenu njema    W:  Mliyoifanya.     K:  Twamwomba na huko      ...

247. Namwandama Bwana

1. Namwandama Bwana    kwa alilonena,    njia yangu huning’azia;     nikimridhisha     atanidumisha     taamini nitii pia.           Amini utii njia           pekee ni hii           ya furaha kwa Yesu:           amini ukatii. 2. Giza sina kwangu     wala hata wingu.    Yeye mara huviondoa     woga, wasiwasi,    sononeko, basi;     Huamini natii pia.           Amini utii … 3. Masumbuko yote,     sikitiko lote;    kwa mapenzi hunilipia;    Baa, dhara, dhiki,    vivyo hubariki.     Niamini nitii pia.           Amini utii … 4. Mimi sitajua     raha sawasawa     ila yote Yesu kumpa;    napata f...

248. Neno Lako Bwana ni Imara

1.  Neno lako Bwana ni imara sana;      hilo latuongoza, hilo latufunza. 2.  Adui wabaya wakikaribia,     Neno lake Bwana ni ulinzi sana. 3.  Siku za dhoruba kesha ukiomba;     Neno lake Bwana msaada sana. 4.  Ukiliamini, huenda na amani;     una na furaha: Neno ni silaha. 5.  Ni furaha kweli, na wingi wa mali     Neno lake Bwana kwa wasiokana. 6.  Neno la rehema, tungali wazima;      faraja i papo, tunapoagana. 7.  Tulijue sana Neno lako, Bwana,     hapa tukupende kisha kwako twende.

249. Kwa Kuwa Hutaogopa

1.  Kwa kuwa hutaogopa      ushuhuda wake,      ishara ile msalaba      ndiyo alama kuu. 2.  Kwa kuwa hutaogopa      kusimama naye     utukufu uupokee,      na kuaibishwa. 3.  Kwa kuwa hutauacha      uimara wako,     tetea Jina la Yesu,     usije ogopa. 4.  Kwa kuwa utapitia     kwa njia nyembamba      inua huo msalaba usiaibike. 5.  Nasi twajiweka kwake,     kwa hiyo ishara,      msalaba beba duniani,      mbinguni ni taji.

250. Baba Uliye Mbinguni

1.  Baba uliye mbinguni      tunakuomba kwa mioyo.     Twakuomba kama wana     waombavyo baba zao,     twaamini: Baba yetu      watusikia mbinguni.   2.  Jina lako litakaswe      likitangazwa popote,      walisikiao Neno     walifuate kwa bidii.      Tulitumie vizuri      Jina la Mungu Mwenyezi.   3.  Na ufalme wako uje      kwa mataifa mengine.      Tupe roho na rehema       tuzishike amri zako.      Ufalme wako ukae      katika mioyo yetu.   4.  Utakayo yatimizwe      duniani kama mbinguni.     Shetani, mwili, dunia,     wasituzuie sisi,     kuyatenda mambo mema      na kukutii mpaka kufa.  5.  Utupe leo chakula      chetu cha kututunzia,     tupate a...

251. Moyo Wangu Furahiwa

1.  Moyo wangu furahiwa,      tazama neema ya Bwana     katika mwaka huu.      Tazama mashamba yote     yanavyostawi vizuri,      yakupendeza wewe,     yakupendeza wewe. 2.  Miti yote yachipuka      Yote yatoa maua      yanayong’aa vizuri.     Milima hata mabonde      tena nyika zimepambwa      kupita nguo zote,     kupita nguo zote. 3.  Chore alia hewani,      vichakani kurumbiza     porini ni kulungu.     Pote sauti za wanyama,     Muumbaji azisikia      sifa za hivi vyote,     sifa za hivi vyote. 4.  Mwenyezi Mungu bariki      vyote ulivyoviweka      chini ya mbingu yako.     Na mioyo yetu ing’ae      kwa neema yako nzuri mno     uliyotupa wewe,      uliyotupa wewe...

252. Mungu Twakuimbia

1. Mungu twakuimbia,     tunasifu nguvu zako.    Tunakuangukia     kwa kuona mambo yako.    Ulivyokuwa kale      utakuwa milele. 2. Nchi zote na mbingu,    na majeshi yao yote,     wote wakuimbia.    Hata wingi wa malaika     wakusifu mbinguni    Ee Mungu mtakatifu. 3. Bwana wetu Mungu mkuu    Mtakatifu mwenye enzi,    u shujaa na Mwokozi,    Mbingu, viumbe, bahari     zimeumbwa na wewe,    zote zinakusifu. 4. Duniani popote    watu wako wakusifu,    ni wazee na watoto    wakuimbiao Baba,    wamsifuo Mwanao    na Roho Mtakatifu. 5. Bwana uturehemu,     utupe baraka yako.    Neema yako iwe kuu,    kwao wakuogopao.    Tunakutumaini,    hivi hatupotei!

253. Nakuimbia Wewe Bwana

1. Nakuimbia wewe Bwana     hakuna mwingine kama wewe.    Nakuimbia nyimbo zangu,     unipe nguvu ya roho wako,    anifundishe nyimbo za sifa,    niziimbe kwa Jina la Yesu. 2. Baba nivute kwa Mwanao,    Mwanao anivute na kwako.    Mtakatifu uniongoze,    mawazo yangu yawe mazuri.    Amani yako ikae mwangu,    nikuimbie kwa furaha kuu. 3. Ukinisaidia hivi,    Bwanangu nitaweza kuimba    kukusifu wewe vizuri    kwa roho na kwa kweli kila saa.    Maana Roho anaongoza     niimbe malaika waimbavyo. 4.  Naomba nilivyofundishwa       na Roho wako yakupendeze.     Nawe unasikia yote      sababu ya Mwana wako Yesu,     aliyenifanya mtoto wako     na mrithi wa ufalme wa mbingu. 5.  Ni heri nikijua haya!     Naweza kukuomba vizuri:     Najua ...

254. Ninataka Kumwimbia Mungu

1.  Ninataka kumwimbia      Mungu kwa furaha kuu.     Ninaona kila siku      anihurumiavyo.     Moyo wake mwenye kweli     umejaa upendo tu,     abariki kwa wingi      wamtumikiao vema.            Vitu vyote vyaisha,            pendo lake milele. 2.  Kama kuku alindavyo      watoto hatarini,      vivyo Baba anilinda     kila siku kwa nguvu.      Ndiye aliyeniumba      akanipa mwili huu     na uzima na roho      siku zote mpaka leo.            Vitu vyote … 3.  Jinsi hii aliupenda     Mungu ulimwengu huu,      hata akamtoa Mwana,      kwa ajili ya watu.     Naye Yesu aliteswa      akafa pale mtini     atuokoe sisi.     Tazame...

255. Tuwe na Raha Moyoni

1.  Tuwe na raha moyoni      na kujazwa shukrani,      kwani Baba wa mbinguni     atutaja watoto.           Daima tutafurahi,           kila siku ni jua.           Njia ya uzima nzuri            sana, tufurahi milele!  2.  Mungu anatuongoza      ni tegemeo letu,      huruma yake hutupa      nguvu ya kila siku.             Daima tutafurahi … 3.  Tunapojitenga naye,     giza latuzunguka,      mwendo wetu si imara      hamna raha moyoni.             Daima tutafurahi …  4.  Waongofu huchipushwa,      njia zao mwanga tu.     Na tumtumikie Yesu      Tukatae kukosa.               Daima tutaf...

256. Njooni Tumsifu Mungu

1.  Njooni tumsifuni Mungu      aliye Mwenyezi,     Mfalme wa popote      mbinguni na duniani.     Kwa sauti kuu     wote wamsifu Mungu,      kumpigia Mfalme shangwe. 2.  Njooni tumsifuni Mungu     anayetawala,      vyote vizuri      akuongozaye na wewe.     Waruka juu     kama kwa nguvu ya tai,     ukiongozwa na Mungu. 3.  Njooni tumsifuni Mungu     aliyetuumba     aliyetupa uzima     na wingi wa neema.      Shida nyingi      zimefukuzwa kwetu,     na Mungu mwenye rehema. 4.  Njooni tumsifuni Mungu      aliyetulinda,     atubariki kwa pendo,      atupa riziki.     Ni Mwenyezi,     atutendea makuu,     anatupenda kwa kweli. 5.  Njooni tumsifuni Mungu,     tumsifu kwa nyimb...

257. Haya ee Moyo Wangu

1. Haya ee moyo wangu,     imba kwa furaha.    Umwimbie Muumbaji     mbingu na dunia.     Atukuzwaye pote     umsifu na wewe    kwa nguvu zako zote,     umri wako wote. 2. Mungu wake Yakobo,     ndiye Mungu wetu.    Ukimchagua yeye,    una fungu jema,     unacho kitu chema,     umepata mali;    moyo utakung’aa     shida zitakwisha.   3. Ni mwenye nguvu nyingi,    hana amshindaye,    kwa hekima aumba,     vyote ni ajabu,     misitu na mabonde,     milima, mashamba,     vilivyo baharini     wanyama porini. 4.  Ana mizungu mingi,      kuponya wanawe.      Anawapa riziki,     hata siku za njaa.     Wenye chakula haba      wanenepa miili: ...

258. Namtumaini Bwana Tu

1. Namtumaini Bwana tu     ndiye mtuliza moyo.    Amkimbiliaye huyu,     hatindikiwi nuru,    Kwa Neno la Bwana Mungu     roho itatulia,    moyo watengemana. 2. Kila anayekupenda    huona msaada wako,     akishikwa na mashaka,    utamtuliza moyo.    Moyoni mwa mpenda Mungu    hamu itatulia,     uchungu hutoweka. 3. Roho yangu usiache    kumtumaini Bwana!    Waelekevu huona;     kwake vituo vyema.    Bwana ndiye mwenye nguvu    katika shida zote;    ni kinga hatarini. 4. Mkononi mwako naweka     maisha na uzima.    Nakuinulia macho     niwapo duniani.    Baada ya siku hizi     ukanipe kukaa     mbinguni kwako Baba.

259. Yesu ni Rafiki Yetu

1. Yesu ni rafiki yetu     akaaye mbinguni.     Hutuombea kwa Baba,     na kutupatanisha,    lakini twajikosesha,    twajitwika mabaya,     tusipomtafuta Yeye     na kuomba kwa kweli. 2. Ukijaribiwa sana     ukiona mashaka,     usihangaike sana,     usikome kumwomba.     Yeye ni mwema kabisa     wa kutuhurumia,     atujua: Tu wanyonge;     husikia kuomba. 3. Ukipatwa na majonzi,     yakulemee sana,    moyo ukisikitika,    Yesu akusikia.    Watu wakikusimanga,     urushwe na dunia,    Yesu akukumbatia;     husikia kuomba! 4. Urafiki haukomi     kwao wampendezao.    Kwa hiyo na tujikaze kumpenda    Bwana Yesu.     Bwana Yesu ndiye Mfalme     awa...

260. Umsifu Mungu ee Roho Yangu

1. Umsifu Mungu ee roho yangu!    Nitamsifu kila siku.    Siku nikaazo duniani    nitamwimbia Bwanangu.     Kanipa mwili na roho,     amestahili sifa kuu.    Haleluya! Haleluya! 2. Wafalme wa humu duniani     ni watu wanaokufa.    Baada ya kufa mashauri     yao yanavunjika kabisa.     Hakuna msaada kwa watu,    Mungu wa juu ndiye mponya.    Haleluya! Haleluya! 3. Asaidiwaye na Mungu Baba     ni mwenye shangwe za kweli.    Huyu haachi kumtegemea,     ijapo shida zizidi.     Aongozwaye na Bwana,    hakosi njia ya msaada.    Haleluya! Haleluya! 4. Ndiye aliyeviumba vyote,     vilivyo juu hata chini.    Shauri la Mungu    linatendeka kila atufanyialo.    Ni Mfalme wa ulimwengu,    atawalaye vizuri!    Haleluya!...

261. Sifuni Bwana

1.  Sifuni Bwana      watoto kwa furaha!      Anasikia      nyimbo zetu watoto.     Sababu hii mwimbieni!   2.  Twapenda sana,      kupaza sauti zetu,      kukuimbia     tena kukushukuru,      tunaokaa duniani.  3. Unasikia watoto waimbao,    nasi twaomba:     utupeleke kwako,     tukusifu na malaika. 

262. Tumshukuru Mungu

1.  Tumshukuru Mungu     kwa kinywa na kwa moyo,     atendaye makuu      popote hata kwetu.      Tangu kuzaliwa      mpaka leo hivi na siku      zijazo hutuhurumia.   2.  Baba mwenye nguvu      atupe siku zote mioyoni mwetu     furaha na amani.     Baraka yake kuu itusaidie,      tushinde huzuni na shida zozote.   3.  Tumsifu Mwenyezi      aliye Baba yetu,      Tumsifu na Mwana aliyetuokoa.      Tumsifu na Roho      atutakasaye.       Tumsifuni Mungu       sasa na milele. 

263. Bwana Wetu Aliye Mwema

1. Bwana wetu aliye mwema,    tunamshukuru!     Haya tumshukuruni milele!          /: Haya tumshukuru. :/   2. Yesu Kristo, Mwokozi wetu,    katuokoa    makosa yetu yote yatoke.        /: Haya tumshukuru. :/ 3. Umshukuru na roho yangu,    kwa mema yote     aliyokutendea bure tu.        /: Haya tumshukuru. :/  4. Atupenda na kutulinda,     siku zozote    Yeye ni Mchungaji wetu wema.        /: Haya tumshukuru. :/

264. Njooni Tuimbe Wimbo Huu

1.  Njooni tuimbe wimbo huu:     Atupenda!     Mungu ni mwenye huruma      Atupenda!      Mliolala  amkeni,     mumtafuteni Mwokozi!      Woga wa kufa uishe!          /: Atupenda! Atupenda!:/            Njooni tuimbe wimbo             huu:  Atupenda! 2.  Utume mwema ndio huu:      Atupenda!     Alitujia toka juu, atupenda!     Mwanawe Mungu, Mwokozi,      atuita sote: Njooni!       Mlioshindwa na mwovu.               Atupenda! Atupenda!..  3.  Ametufia Golgota,      atupenda!     Katupatia uzima, atupenda!     Mponya ni jua la watu,      Yeye ni ngao vitani.     Tumtafuteni kwa bidii.           ...

265. Mganga Wetu ni Karibu

1.  Mganga wetu ni karibu,     hashindwi na uchawi,      upendo wa kutufia     ni dawa yake njema:           Imbeni na malaika,           Jina lenye furaha,          ndilo la kutukuka,            Jina lake Yesu. 2.  Hatuna utengamano      wala uzima hata,     ila Yeye kweli ndiye       aliyetupumzisha:            Imbeni … 3.  Machukio na ugomvi      ametuondolea,     twende na kumtegemea      hata kwake mbinguni:           Imbeni … 4.  Hulioni Jina tamu     lake Mwokozi Bwana?      Atuletea wokovu,     hatashindwa na kufa:            Imbeni … 5.  Hilo ndilo nipendalo,      linipalo uzima, ...

266. Pote Atawala Nani?

  1. K: Pote atawala nani?  W: Pote atawala nani?  K: Ni nani?  W: Ndiye Mungu Mwenyezi. 2. K: Msifuni Mungu wetu,  W: Msifuni Mungu wetu  K: Yu Bwana,  W: Vyote ni mali yake. 3. K: Mwumba jua nao mwezi,  W: Mwumba jua nao mwezi?  K: Na nyota  W: Kwani anayo enzi. 4. K: Sasa wewe roho yangu,  W: Sasa wewe roho yangu  K: Kubali,  W: Nyenyekea kwa Mungu. 5. K: Roho isiyotulia,  W: Roho isiyotulia,  K: Na Bwana,  W: Haitapata raha. 6. K: Amemtuma Mwana wake,  W: Amemtuma Mwana wake,  K: Yesu Kristo,  W: Ili atuokoe. 7. K: Amemshinda shetani,  W: Amemshinda Shetani,  K: Na dhambi,  W: Na kutupa uzima. 8. K: Asimamisha agano  W: Asimamisha agano,  K: La Bwana, W: Haleluya, ee Yesu. 9. K: Dunia wamsifu,  W: Dunia wamsifu  K: Kwa shangwe,  W: Kwa kuwa hututunza. 10. K: Watawala na raia,  W: Watawala na raia,  K: Na waje,  W: W...

267. Baba Yetu Aliye Mbinguni Amenifurahisha

1.  Baba yetu aliye mbinguni      amenifurahisha kwa kweli.     Kaniambia rohoni mwangu     Yesu yu nami, ananipenda.            Anipenda Yesu Mwokozi,            anipenda, anipenda.            Anipenda Yesu Mwokozi,            anipenda kweli. 2.  Nimwachapo nikaenda mbali,      Yeye yu vivyo, ananipenda.     Akaniita kwake upesi,     Yesu yu nami, ananipenda.               Anipenda … 3.  Anipenda, nami nampenda     wokovu wangu ulipokuja.      Tukimwona kufani Golgota,     Yesu yu nami, ananipenda.               Anipenda … 4.  Kujua haya kwanipa raha,     kumtegemea kuna furaha.     Amfukuzapo hivi Shetani,     Yesu yu nami, ananipenda. ...

268. Msingi wa Kanisa

1.  Msingi wa Kanisa      ndiye Yesu Bwana;      kiumbe kipya chake,      alipenda sana; kutaka litafuta      alishuka chini, naye kwa kuja     kwake akafa mtini. 2.  Lina kila taifa, kisha ndilo moja,     wokovu wake una      Mwokozi mmoja;      Uzazi ni mmoja, na moja imani,     chakula ni kimoja, moja tumaini.   3.  Watu hustaajabu      kwa mashaka mengi      yawapatayo nje hata ndani pia.     Ila watakatifu huomba,     wakesha usiku ni kilio,     asubuhi raha. 4.  Mashaka na taabu      hata vita vyake,     vyangoja matimizo      ya amani yake,     ndipo kwa macho yetu      tuone utukufu     Kanisa lishindalo litastarehe juu. 

269. Ni Wako Wewe, Nimekujua

1.  Ni wako wewe, nimekujua     na umeniambia:      Lakini Bwana, nataka kwako     nizidi kusogea:           Bwana vuta, (vuta)           nije nisogee sana           kwako mtini.           Bwana vuta,           vuta nije nisogee           pa damu ya thamani. 2.  Niweke sasa nikatumike     kwa nguvu za neema.      Uyapendayo nami nipende      nizidi kukwandama:           Bwana vuta … 3.  Nina furaha tele kila saa      nizungumzapo kwako,       nikuombapo, nami napata       kujua nia yako:            Bwana vuta, … 4.  Mapenzi yako hayapimiki     ila ng’ambo yaliko      anasa pia si...

270. Mshukuruni, Mshukuru Bwana

1.  Mshukuruni, mshukuru Bwana     kwa kuwa mwema      rehema zake ziko milele,      zadumu milele, zadumu milele. 2.  Kamsifuni, kamsifu      Bwana, ee roho yangu,      usisahau aliyotenda,      aliyokutenda, aliyokutenda 3.  Enzi yake,  enzi ya Bwana     mwenye hekima,     na neema yake isiyokoma,      ni isiyokoma, ni isiyokoma. 4.  Bwana ni Mkuu!     Na Jina lake, ni takatifu      dunia yote imtukuze Ye,     imtukuze Yeye, imtukuze Yeye! 

271. Baba Yetu Uliye Mbinguni

1.  K:  Baba yetu uliye mbinguni,     W:  Jina lako litukuzwe     K:  Ufalme wako uje           mapenzi yatimizwe     W:  Jina lako litukuzwe. 2.  K:  Hapa duniani          kama mbinguni,     W:  Jina lako litukuzwe.       K:  Utupe leo hii riziki yetu.     W:  Jina lako litukuzwe 3.  K:  Utusamehe Baba,          makosa yetu,     W:  Jina lako litukuzwe.     K:  Kwa jinsi sisi nasi           tunavyosamehe.      W:  Jina lako litukuzwe. 4.  K:  Usitutie kamwe          majaribuni      W:  Jina lako litukuzwe.      K:  Bali utuokoe katika            uovu      W:  Jina lako litukuzwe...

272. Twakuomba, ee Baba Mungu

K:  Twakuomba, Ee Baba Mungu,     tupe rehema ya kimbingu;     Tuwe watu wa Mungu. W:  Wa utukufu. 1.  W:  Baba yetu uliye mbinguni,          Jina lako tutalitukuza,         mapenzi yako ni ya makini          mbinguni na duniani. 2.  K:  Tupe leo riziki yetu,         tusamehe makosa yetu          kama sisi tunavyosamehe           wanaotukosea.    3.  W:  Usitutie majaribuni,          Tuokoe na yule mwovu,          kwani wako ndio ufalme          sasa na hata milele.  K:  /: Utukufu ni wako  W:  Hata milele:  K:  Utukufu ni wako  W:  Hata milele.  K:  Utukufu ni wako  W:  Hata milele. K:  Utukufu milele  Amen:/

273. Ewe Baba Yetu

1. Kumtegemea Mwokozi    kwangu tamu kabisa;    kukubali Neno lake,    nina raha moyoni.          Yesu, Yesu namwamini,          nimemwona thabiti;         Yesu, Yesu yu thamani;          ahadi zake kweli.   2. Kumtegemea Mwokozi    kwangu tamu kabisa;    kuamini damu yake,    nimeoshwa kamili.           Yesu, Yesu ... 3. Kumtegemea Mwokozi     kwangu tamu kabisa;    kwake daima napata     uzima na amani.            Yesu, Yesu ...  4. Nafurahi kwa sababu     nimekutegemea,     Yesu, mpendwa na rafiki    uwe nami daima.           Yesu, Yesu ...

274. Ewe Bwana Ndiwe Mchunga

1.  Ewe Bwana ndiwe      Mchunga wangu mwema.     Sitapungukiwa na kitu,      kwani u pamoja nami. 2.  Wanilaza kwenye      malisho tele;      Wanitangulia vizuri,     kwani wanipenda sana. 3.  Nafsi yangu      imehuishwa nawe,     na kuongozwa kwa haki,     kwa ajili ya Jina lako. 4.  Nikipita hata      bonde la mauti,      sitayaogopa mabaya,     kwani Wee u gongo langu. 5.  Umeandaa meza      mbele yangu mimi,     ili na watesi waone,      kwamba ndiwe mwenye neema. 6.  Kichwa changu      kimepakwa na mafuta,     Kombe langu linafurika;      Haya umefanya yote. 7.  Wema wako     umenifuata hasa.     Nami nitaishi na wewe,     kwako, Bwana siku zote. 

275. Tumwimbie Bwana

1.  K:  Tumwimbie Bwana,     W:  Maana ndiye,          mwamba wa wokovu           wetu. 2.  K:  Tuje mbele zake,      W:  Tumfanyie          Yeye shangwe kwa          Zaburi. 3.  K:  Bwana ndiye Mungu      W:  Na Mfalme           Mkuu juu ya miungu            yote. 4.  K:  Mkononi mwake,      W:  Yamo mabonde          na milima ya dunia. 5.  K:  Bahari ni yake,     W:  Aliiumba          pamoja na nchi kavu. 6.  K:  Njooni tumwabudu,      W:  Tumpigie          magoti aliyetuumba. 7.  K:  Ndiye Mungu wetu,      W:  Na sisi ndio         w...

276. Nina Haja Nawe

1.  Nina haja nawe kila saa;      Hawezi mwingine kunifaa.          Yesu nakuhitaji            vivyo kila saa!            Niwezeshe, Mwokozi             nakujia. 2.  Nina haja nawe; kaa nami,     na maonjo haya, hayaumi.            Yesu nakuhitaji … 3.  Nina haja nawe, kila hali,     maisha ni bure, ukiwa mbali,            Yesu nakuhitaji … 4.  Nina haja nawe, nifundishe     na ahadi zako zitimize.            Yesu nakuhitaji … 5.  Nina haja nawe, mweza yote,     ni wako kabisa siku zote.             Yesu nakuhitaji …

277. Leo Siku ya Mungu

1.  Leo siku ya Mungu,     tuko mbele zake.      Jambo kubwa tuabudu      na kusujudia.          /: Sasa tutulie         mbele zake Mungu.         Awe nasi sote         mioyoni mwetu. :/ 2.  Sisi viumbe vyake      tuombe huruma,      Muumba vitu vyote      atuhurumie.           /: Yeye atupenda           na kujua yote.           Manza zetu zote           atazisafisha. :/ 3.  Neno lake la leo      liwe ndani yetu.      Mapenzi yake yote      yatimizwe kwetu.          /: Tumfuate yeye,           na tuishi naye.           Awe baba yetu  ...

278. Mshangilie Bwana

1. K: Mshangilie Bwana dunia yote, mshangilie  W: Bwana dunia yote. 2. K: Msifu Bwana na shangwe kubwa, msifuni  W: Bwana na shangwe kubwa. 3. K: Njooni mbele zake kwa nyimbo nzuri; njooni mbele  W:Zake kwa nyimbo nzuri. 4. K: Jueni kwmba Bwana ndiye Mungu, jueni  W:Kwamba Bwana ndiye Mungu. 5. K: Ndiye Muunba wetu, sisi watu wake; ndiye Muumba  W: Wetu, sisi watu wake. 6. K: Malishoni mwake atuongoza; malishoni  W: Mwake atuongoza. 7. K: Ingieni mwake kwa kumshukuru; ingieni  W: Mwake kwa kumshukuru. 8. K: nyuani mwake tumsifu sote; nyuani  W: Mwake tumsifu sote. 9. K: Na jina lake tulihimidi; na jina  W: Lake tulihimidi. 10. K: Bwana ndiye mwema siku zote kwetu, Bwana ndiye  W: Mwma siku zote kwetu. 11. K: rehema zake ni za milele; rehema  W: Zake ni za milele. 12. K: Uaminifu wake kwa vizazi vyote; uaminifu  W: Wake kwa vizazi vyote.

279. Haleluya, Mshukuruni Bwana

1. Haleluya, mshukuruni Bwana    kwenye kusanyiko la kweli.    Na malaika waungana nasi    kushukuru amani yake.    Matendo yako, Bwana,     ni makubwa kwa wote,         Kazi (Zakutukuza mno          zina utukufu)           zakutukuza (mno ee)          Bwana. 2. Haleluya, mtukuzeni Bwana,    takatifu Jina la Bwana,     wateule duniani pote,     shangilieni upole wake.     Huruma zako Bwana,    ni kubwa kwa wanao.           Kazi … 3. Nchi zote, pokeeni neema,    wokovu huu kwa watu wote.    Kila mtu asikosekane    kwenye lango la mji ule.     Tukiitwa majina,     tutaruka kwa shangwe.            Kazi ...

280. Haleluya, Wote Msifuni Bwana

1. K:  Haleluya,          wote msifuni Bwana     W:  Haleluya,      K:  Haleluya.         Lisifuni Jina lake.     W:  Haleluya,    K:  /: Haleluya,     W:  Haleluya,         Haleluya, Haleluya.     K:  Haleluya,    W:  Haleluya,         Haleluya, Haleluya.:/ 2. K:  Haleluya,         Jina na lihimidiwe,    W:  Haleluya.    K:  Haleluya,         Tangu leo na milele     W:  Haleluya    K:  Haleluya. … 3. K:  Haleluya,         Tangu kucha hata         kuchwa,    W:  Haleluya,     K:  Haleluya,          Jina lake hu...

281. Kwa Nini Wataka Kungoja?

1. Kwa nini wataka kungoja?    Ondoka upesi ndugu!     Mwokozi apenda kukupa    pumziko na raha yake.          Mbona? Mbona?          Mbona hutaki kumjia?          Mbona? Mbona?          Mbona hupendi raha? 2. Ni faida gani kungoja?     Maisha yapita hima.    Ni Yesu tu abarikiye,     kumshika yafaa sana.          Mbona? … 3. Huvutwi moyoni ee ndugu,    na roho yenye uzima?    Hupendi kupata wokovu?     Hima umtafute Yesu.           Mbona? … 4. Kwa nini wataka kungoja?    Kufa kwako ni karibu.     Milango ya mbingu i wazi,     njoo mfuate Yesu Bwana.           Mbona? …

282. Mimi Mkosaji Nakuomba

1.  Mimi mkosaji nakuomba      Mungu wangu Mtakatifu:      Uniendee kwa upole,     nisipotee kabisa.     Uliye na huruma kuu,     Mungu, unihurumie! 2.  Naona hofu kubwa sana      kwa ajili ya makosa.      Nisaidie kwa rehema,      niliye mwenye ubaya.      Uliye na huruma … 3.  Unisikie Baba yangu,      nikikulilia sasa.     Yaondoe makosa yangu,      moyo upate kupoa.     Uliye na huruma … 4.  Usinitupe kwa ukali      kama nilivyostahili.      Unikubali tena, Baba,      katika kundi la wana.      Uliye na huruma … 5.  Ni neno hili liwezalo      kunipa tena moyo mkuu;     “Makosa yameondolewa      Nawe usikose tena”     Uliye na huruma … 6.  Najua umenisikia,     sio...

283. Bwana Yesu Wapi?

1.  Bwana Yesu yuko wapi,     mpenzi wangu rafiki?      Njia gani amekwenda?      Nitamwonaje mimi?      Roho yangu yajutishwa     na dhambi na huzuni;      Yesu mpenzi wangu mwema      namtafuta kwa bidii. 2.  Ninapaza sauti yangu      nalia: Wapi Yesu?      Ndani mwangu sina raha     mpaka nimwone Yesu.      Ningekuwa na mabawa      ningeruka upesi     milimani, mabondeni     kumtafuta Bwanangu. 3.  Aondoa shida zangu,      maharibifu yote.      Nikiona taabu mimi      anituliza yeye.     Nitafanya bidii sana;     kumtafuta popote;      sitachoka kutembea      mchana hata usiku. 4.  Bwana Yesu nitokee,     roho inakuita.      Niondoe na maovu      Yes...

284. Ninakulilia Mungu

1.  Ninakulilia Mungu      katika shida kubwa.      Usikilize maombi     na sala kwa rehema.      Kwani ukiyahesabu      makosa yetu na dhambi,     aponaye ni nani? 2.  Inatupasa rehema      tuondoshwe mabaya.     Kutenda kwetu ni bure,     tujapofanya mema.      Hakuna anayeweza       kujisifu mbele yako,     wataka tu huruma. 3.  Sababu hii inanifaa     kumtumaini Mungu;      rehema yake ni kubwa     aliyoniwekea.     Nashika Neno lake tu      lenye tulizo kubwa mno;     Mungu ana rehema. 4.  Nikiwa na shida nyingi      sababu ya makosa.     Sishindwi nazo, siachi      kumtumaini Mungu.     Wakristo wa kweli wote      wanafuata njia hii,      kungoja saa ya Mun...

285. Nilikuwa Kondoo

1.  Mimi ni mtu mkosaji,      ni mwenye moyo mnyonge,     mwenye uchafu mwingi.     Mungu nihurumie! 2.  Wema sina kabisa,     lakini maovu tu,      nimepunguka sana.     Mungu nihurumie! 3.  Moyo umevunjika,     nina woga kwa macho      kutazama mbinguni.      Mungu nihurumie! 4.  Yuko mmoja mbinguni,      ndiye mwokozi wetu,       nami ninamngojea.      Mungu nihurumie! 5.  Niliyemtegemea,      Yeye hatanitupa,      anipenda kwa moyo.     Mungu nihurumie! 

286. Mimi ni Mtu Mkosaji

1. Mimi ni mtu mkosaji, ni mwenye moyo mnyonge, mwenye uchafu mwingi. Mungu nihurumie! 2. Wema sina kabisa! Lakini maovu tu, nimepunguka sana. Mungu nihurumie! 3. Moyo umevunjika, nina woga kwa macho kutazama mbinguni. Mungu nihurumie! 4. Yuko mmoja mbinguni, ndiye mwokozi wetu, name ninamngojea. Mungu nihurumie! 5. Niliyemtegemea, Yeye hatanitupa, anipenda kw amoyo. Mungu nihurumie!

287. Mwamba Wangu wa Kale

1.  Mwamba wangu wa kale,     kwako nitajificha.      Maji na damu yako     toka mbavuni mwako      ziwe dawa ya dhambi,      kutakasa mioyo. 2.  Si kazi ya mikono      iletayo wokovu.      Nikitoa machozi,      nikifanya na bidii     siwezi kujiosha,      unioshe wewe tu. 3.  Mkononi sina kitu,     ila msalaba wako,     ni mtupu, nipe nguo;     ni mnyonge, nipe nguvu;     niondolee taka,      nitakase sijafa. 4.  Nikaapo duniani,     nifikapo kifoni,      nitakapofufuka,      nitakapokuona;     Mwamba wangu wa kale,     kwako nitajificha!

288. Masikini Bartimayo

1.  Masikini Bartimayo      alikaa njiani,      alikuwa  akiomba      haja za kimwili.   2.  Akasikia sauti kuu      ya jeshi la watu,      akauliza upesi:       Kuna nini ndugu?   3.  Ndiye Yesu Mnazareti,      anapita sasa.     Papo hapo Bartimayo      akaita sana.   4.  Ee Yesu, mwana Daudi,     mimi nakuomba,      sasa unihurumie     kipofu, masikini! 5.  Bwana Yesu kwa huruma     akamwita aje.  Sema:     Watakani kwangu?       Nikufanyieje?  6.  Mimi Bwana ni kipofu,      nataka nione,     nakuomba sana Bwana      unihurumie!  7.  Na Yesu akamwambia:      Nenda zako sasa.      Imani inakuponya!      Mara akaona.  8....

289. Yesu Ndiwe Mponya Wetu

1. Yesu ndiwe Mponya wetu,    ninakukimbilia,    kwani simba hutafuta     atakavyotumeza. 2. Yesu kukutumaini,    kunanipa moyo mkuu,    nina shangwe nikuone     katika ufalme juu. 3. Yesu wewe nakushika,    ijapo kwa unyonge,     kwa mwingine sina msaada,     nikubali, ee Yesu! 4. Yesu nisafishe roho,    nipate kuja kwako,     wema wote niuone     na nikusujudie.

290. Wakosaji Fikirini

1.  Wakosaji fikirini      mwisho wa njia zenu!      Hamwogopi kupotezwa      vibaya kuzimuni?           Rudini kwake Mwokozi!           Ndiye mwenye huruma,           hawatupi wamjiao,             njooni tu kwake Yesu! 2.  Hapo mlipoyafuata     mambo ya dunia hii,     hamkuweza kuvivunja      vifungo vya Shetani.          Rudini kwake … 3.  Mambo yote hugeuka,      tukimjua Mwokozi;     twaondolewa makosa,      tuwe wake Bwana tu.            Rudini kwake … 4.  Wote wampendao Bwana     huwagawia mema;     njooni nanyi myapokee      hayo mema ya mbingu!             Rudini kwake … 5.  Mpokeeni mioyoni...

291. Yesu Awakubali Wakosa

1.  Yesu awakubali      wakosa, wahalifu.     Waambieni wa mbali      habari ya wokovu.             Tangazeni kwa bidii,             akubali wakosa!             Liwe neno dhahiri,             akubali wakosa! 2.  Awakubali Bwana     Neno lake amini,      watu kila aina,     waje kwake tengoni.             Tangazeni …   3.  Mimi ni safi moyo     na mbele ya sheria.     Aliye safi roho      kwake ilitimia.             Tangazeni … 4.  Akubali wakosa,      nami anikubali.      Alivyonitakasa      mbinguni nawasili.             Tangazeni …

292. Usinipite Mwokozi

1.  Usinipite Mwokozi,      unisikie;     Unapozuru wengine,     usinipite.           Yesu, Yesu unisikie;           Unapozuru wengine,            usinipite. 2.  Kiti chako cha rehema     nakitazama;     Magoti napiga pale,     nisamehewe.             Yesu, Yesu … 3.  Sina wa kutegemea,      ila wewe tu;     Uso wako uwe kwangu;     nakuabudu.              Yesu, Yesu … 4.  U Mfariji peke yako;      Sina mwingine,     hapa duniani pote,      ila wewe tu.              Yesu, Yesu … 

293. Kujua Yesu u Karibu

1. Kujua Yesu u karibu     kwanituliza moyo wangu     na kuona: Macho    yako juu yangu kwaniletea     amani nyingi. Nakusifu. 2. Hatujaona uso wako     wenye upole na rehema,     lakini rohoni tunakujua,     tunafahamu huruma yako     na upendo. 3. Afikiriye mchana kutwa     kukufahamu na kujua,    hupata furaha zisizokoma     kwa kuona: Hakuna aliye     kama wewe. 4. Kuvumilia wakosaji,     kutusamehe kila siku,    kutufurahisha na kutuponya,    kutufariji na kutubariki:    Kazi yako. 5. Utuonyeshe wokovu huu,     wa kutuponya kila siku,    ukaifundishe mioyo yetu     ikutukuze na kukupenda     siku zote. 6. Siku za shida tutulize     kwa kufa kwako msalabani,    tukumbuke vema mateso yako ...

294. Mtumwa wa Yesu Huona

1.  Mtumwa wa Yesu huona     furaha nyingi mno.     Si mtumwa wa unyang’anyi,     ni mtoto wa Mungu. 2.  Mtumwa wa dhambi  haoni      njia ya wokovu.     Mtumwa wa Yesu hakosi      njia ya mbinguni. 3.  Mpenda makosa huona      ugomvi na shida.     Watu wa Yesu huona      upendo na raha. 4.  Ubaya wapata kufa,     ni mshahara wake.      Yesu atuokoaye      aleta uzima. 5.  Bwana, umenikomboa      nami nakupenda,      nakutumikia wewe      simtaki mwingine. 6.  Nakuomba Bwana Yesu,     unipeleke juu;     ulipo ndipo pazuri      pa mtumishi wako.

295. Mungu Amenihurumia

1. Mungu amenihurumia,     tendo hili kubwa sana.     Sikustahili jambo hili     nimelipata bure tu.          /: Sasa najua haya yote,/:           nasifu huruma yake.:/  2. Nalistahili kupotea,     lakini nahurumiwa.     Mungu amenipatanisha     na Yeye kwa Yesu Kristo.          /: Hivi vyote vyatoka             wapi?:/          /: Nasema ni huruma              tu:/  3. Jambo hili lenye huruma     nitalisifu daima.     Nalihubiri siku zote,     nikiulizwa na watu.         /: Ndilo furaha yangu           kubwa,:/          /: nalingojea, nikifa. :/  4. Huruma hii ni kubwa sana,   ...

296. Sikiliza Ewe Mtu mkosaji

1.  Sikiliza ewe mtu mkosaji      hutaweza kuyafuta makosa.          /: Yesu ndiye tu          (awezaye kufuta)           Awezaye tu (kuondoa             dhambi zako kabisa)             makosa.:/   2.  Tu wanyonge hata nguvu     hatuna      hatuwezi kujiosha makosa            /:Yesu ndiye tu … :/ 3.  Njooni kwake mpokee      msamaha      damu yake yatuosha      makosa.          /:Yesu ndiye tu … :/  4.  Njia yako ee Bwana     Mungu wetu      tusikose kufuata kabisa.         /:Yesu ndiye tu … :/  5.  Usikie wanao wakiomba      tuwezeshe kujishika na wewe.           /:Yes...

297. Kuna Chemchem Itokayo

1.  Kuna chemchemi itokayo      damu ya wokovu.     Chemchemi itendayo makuu      na kutufariji. 2.  Shida zangu zinakwisha      zote kwa damu hii,     kwani Yesu amekufa     kwa ajili yangu. 3.  Mwana Kondoo damu      yako inayo nguvu kuu.     Tupe roho wako Bwana,      Tuwe watu wapya. 4.  Nami mwenye dhambi      nyingi nimekombolewa.     Kwa damu hii ya Mwokozi,     namsifu Yeye tu. 5.  Damu hii inanipa      furaha ya kweli.      Sababu hii nitamsifu      Mwokozi daima.

298. Kwa Huruma Nikubali

1.  Kwa huruma nikubali     Yesu hivi nilivyo      niwe mali yako Bwana     Mwokozi mtakatifu.           Natafuta raha Bwana           nitaona kwako tu.          Nibariki, unilinde           niliye mtoto wako. 2.  Nitakwenda njia zangu      nikikutumaini.     Unishike nisiweze      kukuacha daima.     Natafuta raha            Bwana… 3.  Nikiona giza tupu     nipe nuru ya roho.      Niongoze kwenye giza     mwenye kweli na nuru.      Natafuta raha             Bwana… 4.  Nitakupa moyo wangu,      nitaishi na wewe,     mpaka macho yawezapo     kuona uso wako.      Natafuta raha          ...

299. Kwako ee Yesu, iko Furaha

1.  Kwako ee Yesu,     iko furaha,      katika shida zote.     Wewe watupa      mambo ya mbingu,     ndiwe Mponya wa kweli.     Watukomboa sisi watumwa.     Akushikaye, atasimama      hata milele, Haleluya!      Tunakumbuka rehema zako,     Tunakushika hata tukifa      hatukuachi, Haleluya! 2.  Tukikushika, mwovu na kufa     hana nguvu juu yetu.      Wewe hodari kutukingia shida     na msiba wote.     Twakutukuza, twakuimbia,      tunazidisha heshima yako     kwa nyimbo nzuri. Haleluya!     Tuna furaha, twashangilia,     twasifu sana nguvu ya Bwana     hatutakoma.  Haleluya!

300. Mimi ni Mwana Kondoo

1. Mimi ni Mwana Kondoo  kikundini mwa Yesu,  ninafurahishwa sana  na Mchungaji wangu  mwema; anipenda kabisa,  anilisha vizuri. 2. Yeye akinilisha,  ninatunzwa vizuri  sina njaa, wala kiu,  sina shida, wala hofu,  ninaona raha tu  na furaha moyoni. 3. Heri yangu ni kubwa  nipendwaye na Yesu,  siku zangu zikiisha,  anipeleka mbinguni  anikumbatiapo  Yesu Mchungaji mwema.

301. Mungu ni Pendo

1.  Mungu ni pendo!      Apenda watu!      Mungu ni pendo      anipenda.            Sikilizeni furaha yangu:           Mungu ni pendo            anipenda! 2.  Nilipotea katika dhambi     nikawa mtumwa wa      Shetani.          Sikilizeni … 3.  Akaja Yesu kunikomboa,      Yeye kanipa kuwa huru.            Sikilizeni … 4.  Sababu hii namtumikia,      namsifu Yeye siku zote.            Sikilizeni … 

302. Mungu Wetu Ndiye Boma

1. Mungu wetu ndiye boma,     silaha tena ngao,     atukingiaye shida    zitushikazo sisi.    Adui wa kale    afanya hila ya kutushinda,    ni mwenye nguvu kuu,     hakuna amwezaye.   2. Nguvu zetu hazifai    tunashindwa upesi.    Lakini tunaye shujaa     aliye mwenye nguvu.     Jina lake nani?    Ni Yesu Kristo    Mungu mwenyewe,    hapana mwingine    ni mshindaji wa wote. 3. Shetani akikusanya     majeshi yake yote.    Hatuogopi kabisa     kwani tutawashinda!    Mfalme wa dunia akunja uso    ana hasira, lakini ni bure:    Neno moja tu lamweza!  4. Neno la Mungu lashinda!    Halitafuti msaada.     Mungu yu pamoja nasi na roho     ya hekima. Wakitunyang’anya     watoto wenzi;  ...

303. Neno Moja Bora Sana

1. Neno moja bora sana,    lishindalo mengine.    Mambo yote ya dunia     ndiyo mzigo mzito tu,    unaotutesa miili na roho,    lakini hayatunyang’anyi furaha.    Nikiwa na moja lililo bora     naona furaha isiyoisha. 2. Roho ukitaka hili,    hulioni kwa watu.    Acha mambo ya dunia,     hima nenda mbinguni,     alipo Mwokozi     pamoja na Mungu,    palipo na nguvu      na haki na kweli,    ndipo utakapoliona lile     linalokupasa hapa na huko.   3. Kumbuka Maria pale     miguuni pa Yesu.     Alivyosikia Neno alilohubiriwa.    Hakuna jingine alilolipenda     kuliko maneno ya     Yesu Mwokozi;     hakuna mawazo aliyowaza    kuliko kumwona na kumsikia. 4. Hivyo hata moyo wangu    ...

304. Nitakupenda Nguvu Yangu

1.  Nitakupenda nguvu yangu      nitakupenda Mwokozi,      nitakupenda nikitenda     mambo yakupendezayo,      nitakupenda nuru kuu,      kwa nguvu za moyo. 2.  Nitakupenda ee rafiki      uzima wangu wa kweli.     Nitakupenda na kusifu,      nionapo mwanga wako.      Nitakupenda, Mwokozi      Kondoo wa Mungu. 3.  Nimechelewa Bwana wangu,     kukufuata vizuri;     sikukujua siku nyingi,      uliye raha ya moyo.      Lakini sasa najuta       nitakufuata. 4.  Nakushukuru jua langu,     waning’aza moyo wangu;      nakushukuru Bwana wangu,     uliyenipa uhuru;      nakushukuru Mwokozi      uliyeniponya. 5.  Unipe nguvu ya kudumu      nisikuache kabisa;     uniongoze siku z...

305. Unishike! Mimi ni Mnyonge

1. Unishike!    Mimi ni mnyonge sana     siwezi kwenda pasipo Wewe.    Unishike!     Uliye Mponya wangu,     hofu na taabu hainishindi. 2. Unishike! Ukanivute kwako,    niwe karibu na moyo wako.    Unishike! Kwani nakosa njia    nzuri nikienda peke yangu. 3. Unishike! Naona giza tupu     nisipouona uso wako.    Lakini nuru yako iking’aza     njia yangu naona furaha. 4. Unishike! Utakaponiita niende    kulazwa kaburini.    Mwanga wako utokao     mbinguni    uning’azie njia ya mwisho.

306. Yesu Hukaribisha

1. Yesu hukaribisha    wenye mabaya! Pasheni     wote waliokosa    Neno hili la faraja,     walisikie vema:    “Yesu ndiye Mwokozi.” 2. Twastahili kufa tu,    Yesu hutuhurumia, akatufungulia    mlango wa rehema kubwa.    Nasi sasa twajua:    “Yesu ndiye Mwokozi.” 3. Akipotea kondoo,    Mchunga mwema amtafuta.    Yesu Mchunga wa watu    anawatafuta wote     waliokosa njia:   “Yesu ndiye Mwokozi.”  4. Yesu hukaribisha    wakosaji, hata mimi     ameniita kwake,     mbingu imefunguliwa.     Naungama nikifa:     “Yesu ndiye Mwokozi.”

307. Yesu Mpenzi Wangu

1. Yesu mpenzi wangu     ufurahishaye    moyo kwa kweli.     Tangu siku nyingi     nina hamu kubwa    nawe Bwanangu.    Ndiwe mpenzi wangu mkuu,    Wewe peke yako Mponya     hapa duniani. 2. Wewe mlinzi wangu     waondoa shida zinitesazo.    Mwovu aogofye,    vyote viteteme,    Yesu yu kwangu.     Huzuni ikizidi,     vyote vikiharibika     Yesu anishika. 3. Nakataa furaha hata mali zote     za dunia hii.    Yesu mali yangu.     Yesu ni furaha ya moyo wangu.    Nikiachwa kabisa    na jamaa zangu wote,     sitamwacha Yesu. 4. Roho ya huzuni     nenda zako mbali, Yesu yuaja.    Yesu akiwapo, hata shida zote     hazinishindi.     Watu wakinitesa    hawawezi kunitenga...

308. Yesu ni Mponya, Anatupenda

1. Yesu ni mponya,     anatupenda,    upendo wake mkubwa sana.    Ametujia atuokoe,    atupe raha na uzima. 2. Akaja kwetu atuokoe,     tusikamatwe na Shetani.    Tusimsahau Mwokozi wetu     tumpende sana Mungu wetu. 3. Atupa nguvu, atusafisha mioyo    yetu itakate.     Tumtumikie Mwokozi wetu,    tumpende sana Mungu wetu. 4. Yesu ni Mponya tumsifu yeye,    Yesu ni mkubwa, tumfuate.    Atupeleke mbinguni kwake,    mbinguni kwake iko raha!

309. Karibu na Wewe, Mungu

1. Karibu na Wewe,     Mungu wangu,     nikukaribie, Bwana wangu.    Siku zote niwe karibu na Wewe,    nikukaribie Mungu wangu! 2. Mimi nasafiri duniani,     pa kupumzikia sipaoni.    Nilalapo niwe    Karibu na Wewe, … 3. Yote unipayo yanivuta,    pa kukaribia nitapata.    Furahani niwe     karibu na Wewe, … 4. Na kwa nguvu zangu     sitakwenda,    sina la kufanya peke yangu.    Mashakani niwe     karibu na Wewe, … 5. Nitakapofika kwako mjini     nitakapokula mkate wako, kwa    milele niwe karibu na Wewe,    karibu kabisa, Mungu wangu!

310. Ewe Mungu Ngome Yetu

1. Ewe Mungu ngome yetu     ya miaka mingi,    Wewe u msaada wetu    na ngao ya nguvu.   2. Chini ya kiti cha enzi     hatutaogopa,    mkono wako wenye nguvu    watusaidia.   3. Miaka elfu waona     kama siku moja,    ndiwe Mungu wa milele,    hukomi kabisa.   4. Maisha yetu yapita    kama maji ya mto,     na rafiki yetu kama     ndoto ya usiku.   5. Ewe Mungu ngome yetu     ya miaka mingi,    zifikishe roho zetu kwako    juu mbinguni. 

311. Neno la Mungu Takata

1. Neno la Mungu takata     lililotoka mbinguni;     ambalo moto na panga     haziwezi kulishinda.     Twakushika siku zote     maishani na kufani. 2. Waliotutangulia     waliokutegemea,    wamekufia mashujaa;     nasi tulio watoto.     Twakushika … 3. Neno la Mungu takata,     tukushuhudie nasi     kwa neno tamu na     tendo kunako wenzi au adui.    Twakushika … 

312. Nakuapia Yesu

1. Nakuapia Yesu kukutumikia    Wewe u mfunzi wangu    na rafiki mwema.     Sitaogopa vita nikikufuata     siipotezi njia ukiniongoza. 2. Dunia i karibu, Bwana unilinde,    na majaribu mengi     yako pande zote.    Adui siku zote ni ndani na nje,     Ee Yesu univute  karibu na Wewe! 3. Nazisikia sauti     zenye tamaa mbaya,     na mambo ya dunia     yanivuta sana.     Ee Bwana sema nami,     furaha iwe kuu,     nitakusikiliza,    Wewe mlinzi wangu. 4. Waagana na wote wakufuatao,    kwamba uliko Wewe,     nao watakuwa.    Nami ninaagana kukutumikia,    Yesu nisaidie  kukuandamia. 5. Hatua zako Bwana     naziona wazi,    nizikanyage vema    hapa duniani.    Nishike hata mwisho,    Ee ...

313. Kwa Neema na Pendo

1. Kwa neema na pendo     ameniweka huru,    si ustahili wangu,    si haki na matendo.         /: Ni Yesu, Bwana          wangu,          Kwa neema ’meniweka          huru./: 2. Kwa moyo wa ubaba    ameniweka huru,    si kwa sababu zangu,    si kwa ujuzi wangu.             Ni Yesu, … 3. Kwa utakaso wake     amesamehe yote;     Amefuta madeni     na dhambi na ujinga.            Ni Yesu, …  4. Kwa damu ya thamani     amelipia yote;    Na vyeti vya madai     amepasua vyote,            Ni Yesu … 5. Kwa ukubali wake     amekubali wote:     Wenye mizigo wote     huwapumzisha vema.      ...

314. Ni Mpweke Hivi

1.  Ni mpweke hivi sina  rafiki.     Mwenzangu Yesu,     Yeye yu nami.     Ananifariji katika njia,     Ananifariji katika njia. 2.  Wenzangu wote, wanichukie,      wakiniacha sitaogopa.      Pendo lake Yesu      ni ngome yangu,     pendo lake Yesu     ni ngome yangu. 3.  Kazini mwangu dhiki napata.      Ingawa hivyo Yesu simwachi.     Ananiongoza na kuhifadhi,     Ananiongoza na kuhifadhi. 4.  Ee moyo wangu usiogope.     Jikaze sasa, Yesu Mwenzio.     Atakuokoa katika shida,     Atakuokoa katika shida. 

315. Bwana ni Nuru na Wokovu Wangu

1.  K:  Bwana ni nuru         na wokovu wangu,      W:  Ni ngome ya uzima wangu,         Nimhofu nani duniani? 2.  K:  Watenda mabaya           walinijia,      W:  Wanile nyama yangu yote,         Wakajikwaa  wakaanguka. 3.  K:  Jeshi likijipanga  tupigane,     W:  Moyo wangu hauogopi,         vita vijaponitokea. 4.  K:  Hata hapo ninalo tumaini;     W:  Neno moja nataka, Bwana,         ndilo ninalolitafuta. 5.  K:  Nikae nyumbani           mwa Bwana wangu,      W:  Siku zote maisha yangu,         nione uso wake Bwana. 6.  K:  Niutazame uzuri           wa Bwana.     W:  Nikae hekaluni mwake,    ...

316. Ati Tuonane Mtoni?

1. Ati tuonane mtoni?    Maji mazuri ya mbingu;    Yanatokea mwangani,     penye kiti cha Mungu.          Naam, tuonane mtoni!          Watakatifu,           kwenu ni mtoni!           Tutakutanika mtoni           penye kiti cha Mungu. 2. Tukitembea mtoni     na Yesu Mchunga wetu     daima tu ibadani    usoni pake kwetu.          Naam, tuonane … 3. Kwang’ara sana mtoni,    cha Mwokozi ni kioo,     milele hatuachani     tumsifu kwa nyimbo.           Naam, tuonane … 4. Si mbali sana mtoni     karibu tutawasili,    mara huwa furahani     na amani ya kweli.           Naam, tuonane … 

317. Cha Kutumaini Sina

1.  Cha kutumaini sina      ila damu yake Bwana,     sina wema wa kutosha     dhambi zangu kuziosha;            Kwake Yesu nasimama,             ndiye Mwamba ni salama             ndiye Mwamba ni salama. 2.  Njia yangu iwe ndefu      Yeye hunipa wokovu;      Mawimbi yakinipiga      nguvu zake ndiyo nanga.              Kwake Yesu … 3.  Damu yake na sadaka      nategemea daima,      yote chini yakiisha     Mwokozi atanitosha.                 Kwake Yesu … 4.  Nikiitwa hukumuni,     rohoni nina amani;      Nikivikwa haki yake     sina hofu mbele zake.                 Kwake Yesu …

318. Niongoze, Bwana Mungu

1. Niongoze, Bwana Mungu     ni msafiri chini;    Ni mnyonge, nguvu sina    nishike mkononi;     U Mkate wa mbinguni,    nilishe siku zote,     nilishe siku zote. 2. Kijito cha maji mema    kitokacho mwambani,     nguzo yako, moto, wingu,    yaongoza jangwani;    Niokoe Mwenye nguvu;    Nguvu zangu na ngao,     nguvu zangu na ngao. 3. Nikikaribia kufa,     sichi neno lolote,     Wewe kifo  umeshinda     zinawe nguvu zote,    tutaimba sifa zako,    kwako juu milele,     kwako juu milele.

319. Yesu Unipendaye

1. Yesu unipendaye     kwako nakimbilia,     ni wewe utoshaye     mwovu akinijia;     yafiche ubavuni     mwako maisha yangu;     Nifikishe mbinguni,     wokoe moyo wangu. 2. Ngome nyingine sina,    Nategemea kwako.     Usinitupe Bwana,    nipe neema yako,     ninakuandamia     mwenye kuniwezesha;     Shari wanikingia,    vitani wanitosha. 3. Nakutaka Mpaji     vyote napata kwako;    Niwapo mhitaji,     utanijaza vyako;    Nao waangukao    wanyonge wape nguvu;     Poza wauguao.    Uongoze vipofu. 4. Bwana umeniosha    moyo kwa damu yako;    Neema ya kutosha     yapatikana kwako;     Kwako Bwana naona,     kisima cha uzima:    mwangu moyon...