252. Mungu Twakuimbia

1. Mungu twakuimbia, 

   tunasifu nguvu zako.

   Tunakuangukia 

   kwa kuona mambo yako.

   Ulivyokuwa kale  

   utakuwa milele.


2. Nchi zote na mbingu,

   na majeshi yao yote, 

   wote wakuimbia.

   Hata wingi wa malaika 

   wakusifu mbinguni

   Ee Mungu mtakatifu.


3. Bwana wetu Mungu mkuu

   Mtakatifu mwenye enzi,

   u shujaa na Mwokozi,

   Mbingu, viumbe, bahari 

   zimeumbwa na wewe,

   zote zinakusifu.


4. Duniani popote

   watu wako wakusifu,

   ni wazee na watoto

   wakuimbiao Baba,

   wamsifuo Mwanao

   na Roho Mtakatifu.


5. Bwana uturehemu, 

   utupe baraka yako.

   Neema yako iwe kuu,

   kwao wakuogopao.

   Tunakutumaini,

   hivi hatupotei!

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu