257. Haya ee Moyo Wangu

1. Haya ee moyo wangu, 

   imba kwa furaha.

   Umwimbie Muumbaji 

   mbingu na dunia. 

   Atukuzwaye pote 

   umsifu na wewe

   kwa nguvu zako zote, 

   umri wako wote.


2. Mungu wake Yakobo, 

   ndiye Mungu wetu.

   Ukimchagua yeye,

   una fungu jema, 

   unacho kitu chema, 

   umepata mali;

   moyo utakung’aa 

   shida zitakwisha.

 

3. Ni mwenye nguvu nyingi,

   hana amshindaye,

   kwa hekima aumba, 

   vyote ni ajabu, 

   misitu na mabonde, 

   milima, mashamba, 

   vilivyo baharini 

   wanyama porini.


4.  Ana mizungu mingi, 

    kuponya wanawe. 

    Anawapa riziki,

    hata siku za njaa.

    Wenye chakula haba 

    wanenepa miili:

    hata waliofungwa 

    anawafungua.


5.  Mashangilio yote,

    hayamtoshi yeye.

    Ni mwema peke yake 

    nami ni vumbi tu!

    Ananihurumia

    kwa kuwa ni wake,

    kwa hiyo nalikuza

    Jina lake pote. 


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

265. Mganga Wetu ni Karibu