Sisi tukusanyikao hapa twapeana mikono tuyakumbuke mateso yako, tusijitenge nawe. Nayo kazi hii ya roho zetu kama inakupendeza Bwana, utujibu: Amen, tutulie mioyo!
Wazima wote wamsifu Bwana, Wazima wote wamsifu Bwana! Msifu Bwana, Msifu Bwana. Nyumbani mwake tumshangilie nguvu zake za juu tuzisifu! Wazima wote, msifu Bwana, wazima wote, wazima wote, Wamsifu Bwana! Wamsifu Bwana! Kwa filimbi na baragumu na vinubi hata zeze na ngoma wamsifu Bwana, wamsifu Bwana. Wazima wote, wamsifu Bwana baragumu na filimbi wamsifu Bwana, Ee, Bwana wa Majeshi. Haleluya.
1. Kristo usituondoke sababu mchana waisha, mwanga wa Neno la Mungu usiuzimishe kwetu! 2. Nyakati hizi za mwisho tusaidie kushika Neno la huruma yako nalo fumbo takatifu. 3. Kundi lako ulilinde ulikusanye mwenyewe, libariki Neno lako, litangaziwe popote! 4. Mambo na mashauri yote si yetu ila ni yako, kwa hiyo wasimamishe wanaokutegemea. 5. Neno lako ngome kubwa, hata boma la makundi; kwa Neno lako tulishe tusitafute mengine!
1. Huruma zako ni nyingi Yesu siku kwa siku, mapenzi yako yapita kiasi cha maneno! 2. Watupenda na kutoa damuyo msalabani, watakatifu wapenda kumwona Mungu wao. 3. Watupenda tangu mwanzo, ni mwanzo wa furaha. Mwisho wa kutegemea ni kukuona wewe. 4. Tujue, Bwana, Mkombozi, utupendavyo sasa mpaka tutakapokufa, tutakuona wewe.
1. K: Wenzetu leo hii twawaaga kweli W: Muende salama. K: Njiani muwe na safari ya heri; W: Mlindwe na Bwana. K: Kweli W: Mfike salama. K: Nyumbani W: Muone jamaa. 2. K: Tunayo huzuni, furaha, sababu W: Ninyi mwatutoka. K: Lakini tunayo imani kwa Mungu W: Kwamba tu pamoja, K: Katika W: Sala za imani. K: Twaona W: Umoja wa kweli. 3. K: Twamsifu Bwana kwa kazi yenu njema W: Mliyoifanya. K: Twamwomba na huko ...
1. Namwandama Bwana kwa alilonena, njia yangu huning’azia; nikimridhisha atanidumisha taamini nitii pia. Amini utii njia pekee ni hii ya furaha kwa Yesu: amini ukatii. 2. Giza sina kwangu wala hata wingu. Yeye mara huviondoa woga, wasiwasi, sononeko, basi; Huamini natii pia. Amini utii … 3. Masumbuko yote, sikitiko lote; kwa mapenzi hunilipia; Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki. Niamini nitii pia. Amini utii … 4. Mimi sitajua raha sawasawa ila yote Yesu kumpa; napata f...