244. Kristo Usituondoke
1. Kristo usituondoke
sababu mchana waisha,
mwanga wa Neno la Mungu
usiuzimishe kwetu!
2. Nyakati hizi za mwisho
tusaidie kushika
Neno la huruma yako
nalo fumbo takatifu.
3. Kundi lako ulilinde
ulikusanye mwenyewe,
libariki Neno lako,
litangaziwe popote!
4. Mambo na mashauri yote
si yetu ila ni yako,
kwa hiyo wasimamishe
wanaokutegemea.
5. Neno lako ngome kubwa,
hata boma la makundi;
kwa Neno lako tulishe
tusitafute mengine!
Comments
Post a Comment