304. Nitakupenda Nguvu Yangu

1.  Nitakupenda nguvu yangu 

    nitakupenda Mwokozi, 

    nitakupenda nikitenda

    mambo yakupendezayo, 

    nitakupenda nuru kuu, 

    kwa nguvu za moyo.


2.  Nitakupenda ee rafiki 

    uzima wangu wa kweli.

    Nitakupenda na kusifu, 

    nionapo mwanga wako. 

    Nitakupenda, Mwokozi 

    Kondoo wa Mungu.


3.  Nimechelewa Bwana wangu,

    kukufuata vizuri;

    sikukujua siku nyingi, 

    uliye raha ya moyo. 

    Lakini sasa najuta  

    nitakufuata.


4.  Nakushukuru jua langu,

    waning’aza moyo wangu; 

    nakushukuru Bwana wangu,

    uliyenipa uhuru; 

    nakushukuru Mwokozi 

    uliyeniponya.


5.  Unipe nguvu ya kudumu 

    nisikuache kabisa;

    uniongoze siku zote 

    nisianguke njiani,

    ung’aze mwili na roho 

    kwa nuru ya mbingu.


6.  Nitakupenda taji yangu 

    nikiwa mwenye furaha; 

    nitakupenda Mponya wangu, 

    huzuni ikinitesa, 

    nitakupenda daima.

    Yesu Bwana wangu. 


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu