254. Ninataka Kumwimbia Mungu

1.  Ninataka kumwimbia 

    Mungu kwa furaha kuu.

    Ninaona kila siku 

    anihurumiavyo.

    Moyo wake mwenye kweli

    umejaa upendo tu,

    abariki kwa wingi 

    wamtumikiao vema.

           Vitu vyote vyaisha,

           pendo lake milele.


2.  Kama kuku alindavyo 

    watoto hatarini, 

    vivyo Baba anilinda

    kila siku kwa nguvu. 

    Ndiye aliyeniumba 

    akanipa mwili huu

    na uzima na roho 

    siku zote mpaka leo.

           Vitu vyote …


3.  Jinsi hii aliupenda

    Mungu ulimwengu huu, 

    hata akamtoa Mwana, 

    kwa ajili ya watu.

    Naye Yesu aliteswa 

    akafa pale mtini

    atuokoe sisi.

    Tazameni pendo hili! 

             Vitu vyote …


4.  Roho wake Mtakatifu 

    ni kiongozi wangu, 

    aniangalia vema 

    niingie mbinguni.

    Aning’aza moyo wangu 

    kwa tegemeo langu 

    limshindalo Shetani,

    asiweze kunidhuru. 

             Vitu vyote …


5.  Nikishikwa na huzuni

    ninajua faraja: 

    Shida na mateso yote

    mwisho yatageuka.

    Baada ya kaskazi kali

    yanakuja masika,

    vivyo baada ya shida

    napewa furaha kubwa. 

            Vitu vyote ...


6.  Pendo lake haliishi

    Neno hili ni kweli.

    Basi mimi mtoto wake

    ninamwomba Babangu:

    Unihurumie mimi, 

    nikushike kwa nia,

    nikupende daima, 

    niishipo duniani;

    na halafu milele 

    nitakaa na wewe.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu