260. Umsifu Mungu ee Roho Yangu
1. Umsifu Mungu ee roho yangu!
Nitamsifu kila siku.
Siku nikaazo duniani
nitamwimbia Bwanangu.
Kanipa mwili na roho,
amestahili sifa kuu.
Haleluya! Haleluya!
2. Wafalme wa humu duniani
ni watu wanaokufa.
Baada ya kufa mashauri
yao yanavunjika kabisa.
Hakuna msaada kwa watu,
Mungu wa juu ndiye mponya.
Haleluya! Haleluya!
3. Asaidiwaye na Mungu Baba
ni mwenye shangwe za kweli.
Huyu haachi kumtegemea,
ijapo shida zizidi.
Aongozwaye na Bwana,
hakosi njia ya msaada.
Haleluya! Haleluya!
4. Ndiye aliyeviumba vyote,
vilivyo juu hata chini.
Shauri la Mungu
linatendeka kila atufanyialo.
Ni Mfalme wa ulimwengu,
atawalaye vizuri!
Haleluya! Haleluya!
5. Yeye apenda kusaidia
wote wateswao bure.
Awashibisha wapate nguvu
wanaoona njaa sana.
Awafungua wafungwa,
anazo rehema nyingi.
Haleluya! Haleluya!
6. Enyi umati sifuni Bwana
awatendeaye makuu.
Wenye uzima wamsifu sana
na mashangilio mema.
Tumwimbiaye ni Mungu
Baba na Mwana na Roho.
Haleluya! Haleluya!
Comments
Post a Comment