293. Kujua Yesu u Karibu
1. Kujua Yesu u karibu
kwanituliza moyo wangu
na kuona: Macho
yako juu yangu kwaniletea
amani nyingi. Nakusifu.
2. Hatujaona uso wako
wenye upole na rehema,
lakini rohoni tunakujua,
tunafahamu huruma yako
na upendo.
3. Afikiriye mchana kutwa
kukufahamu na kujua,
hupata furaha zisizokoma
kwa kuona: Hakuna aliye
kama wewe.
4. Kuvumilia wakosaji,
kutusamehe kila siku,
kutufurahisha na kutuponya,
kutufariji na kutubariki:
Kazi yako.
5. Utuonyeshe wokovu huu,
wa kutuponya kila siku,
ukaifundishe mioyo yetu
ikutukuze na kukupenda
siku zote.
6. Siku za shida tutulize
kwa kufa kwako msalabani,
tukumbuke vema mateso yako
na kukushika kwa nguvu zote
mioyoni.
7. Kwa njia hii tutafurahi
kama watoto mpaka mwisho.
Na ikitupasa kuhuzunika
utufariji mioyo yetu, itulie.
8. Unatuonyesha makovu
uliyopata msalabani.
Nasi tukiona alama hizi
hatuna budi kukushukuru
na kusifu.
Comments
Post a Comment