289. Yesu Ndiwe Mponya Wetu
1. Yesu ndiwe Mponya wetu,
ninakukimbilia,
kwani simba hutafuta
atakavyotumeza.
2. Yesu kukutumaini,
kunanipa moyo mkuu,
nina shangwe nikuone
katika ufalme juu.
3. Yesu wewe nakushika,
ijapo kwa unyonge,
kwa mwingine sina msaada,
nikubali, ee Yesu!
4. Yesu nisafishe roho,
nipate kuja kwako,
wema wote niuone
na nikusujudie.
Comments
Post a Comment