281. Kwa Nini Wataka Kungoja?
1. Kwa nini wataka kungoja?
Ondoka upesi ndugu!
Mwokozi apenda kukupa
pumziko na raha yake.
Mbona? Mbona?
Mbona hutaki kumjia?
Mbona? Mbona?
Mbona hupendi raha?
2. Ni faida gani kungoja?
Maisha yapita hima.
Ni Yesu tu abarikiye,
kumshika yafaa sana.
Mbona? …
3. Huvutwi moyoni ee ndugu,
na roho yenye uzima?
Hupendi kupata wokovu?
Hima umtafute Yesu.
Mbona? …
4. Kwa nini wataka kungoja?
Kufa kwako ni karibu.
Milango ya mbingu i wazi,
njoo mfuate Yesu Bwana.
Mbona? …
Comments
Post a Comment