258. Namtumaini Bwana Tu

1. Namtumaini Bwana tu 

   ndiye mtuliza moyo.

   Amkimbiliaye huyu, 

   hatindikiwi nuru,

   Kwa Neno la Bwana Mungu 

   roho itatulia,

   moyo watengemana.


2. Kila anayekupenda

   huona msaada wako, 

   akishikwa na mashaka,

   utamtuliza moyo.

   Moyoni mwa mpenda Mungu

   hamu itatulia, 

   uchungu hutoweka.


3. Roho yangu usiache

   kumtumaini Bwana!

   Waelekevu huona; 

   kwake vituo vyema.

   Bwana ndiye mwenye nguvu

   katika shida zote;

   ni kinga hatarini.


4. Mkononi mwako naweka 

   maisha na uzima.

   Nakuinulia macho 

   niwapo duniani.

   Baada ya siku hizi 

   ukanipe kukaa 

   mbinguni kwako Baba.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu