279. Haleluya, Mshukuruni Bwana
1. Haleluya, mshukuruni Bwana
kwenye kusanyiko la kweli.
Na malaika waungana nasi
kushukuru amani yake.
Matendo yako, Bwana,
ni makubwa kwa wote,
Kazi (Zakutukuza mno
zina utukufu)
zakutukuza (mno ee)
Bwana.
2. Haleluya, mtukuzeni Bwana,
takatifu Jina la Bwana,
wateule duniani pote,
shangilieni upole wake.
Huruma zako Bwana,
ni kubwa kwa wanao.
Kazi …
3. Nchi zote, pokeeni neema,
wokovu huu kwa watu wote.
Kila mtu asikosekane
kwenye lango la mji ule.
Tukiitwa majina,
tutaruka kwa shangwe.
Kazi ...
Comments
Post a Comment