248. Neno Lako Bwana ni Imara
1. Neno lako Bwana ni imara sana;
hilo latuongoza, hilo latufunza.
2. Adui wabaya wakikaribia,
Neno lake Bwana ni ulinzi sana.
3. Siku za dhoruba kesha ukiomba;
Neno lake Bwana msaada sana.
4. Ukiliamini, huenda na amani;
una na furaha: Neno ni silaha.
5. Ni furaha kweli, na wingi wa mali
Neno lake Bwana kwa wasiokana.
6. Neno la rehema, tungali wazima;
faraja i papo, tunapoagana.
7. Tulijue sana Neno lako, Bwana,
hapa tukupende kisha kwako twende.
Comments
Post a Comment