259. Yesu ni Rafiki Yetu

1. Yesu ni rafiki yetu 

   akaaye mbinguni. 

   Hutuombea kwa Baba, 

   na kutupatanisha,

   lakini twajikosesha,

   twajitwika mabaya, 

   tusipomtafuta Yeye 

   na kuomba kwa kweli.


2. Ukijaribiwa sana 

   ukiona mashaka, 

   usihangaike sana, 

   usikome kumwomba. 

   Yeye ni mwema kabisa 

   wa kutuhurumia, 

   atujua: Tu wanyonge; 

   husikia kuomba.


3. Ukipatwa na majonzi, 

   yakulemee sana,

   moyo ukisikitika,

   Yesu akusikia.

   Watu wakikusimanga, 

   urushwe na dunia,

   Yesu akukumbatia; 

   husikia kuomba!


4. Urafiki haukomi 

   kwao wampendezao.

   Kwa hiyo na tujikaze kumpenda

   Bwana Yesu. 

   Bwana Yesu ndiye Mfalme 

   awashindaye wote;

   wote wamtumikiao 

   atawavika taji.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu