299. Kwako ee Yesu, iko Furaha
1. Kwako ee Yesu,
iko furaha,
katika shida zote.
Wewe watupa
mambo ya mbingu,
ndiwe Mponya wa kweli.
Watukomboa sisi watumwa.
Akushikaye, atasimama
hata milele, Haleluya!
Tunakumbuka rehema zako,
Tunakushika hata tukifa
hatukuachi, Haleluya!
2. Tukikushika, mwovu na kufa
hana nguvu juu yetu.
Wewe hodari kutukingia shida
na msiba wote.
Twakutukuza, twakuimbia,
tunazidisha heshima yako
kwa nyimbo nzuri. Haleluya!
Tuna furaha, twashangilia,
twasifu sana nguvu ya Bwana
hatutakoma. Haleluya!
Comments
Post a Comment