267. Baba Yetu Aliye Mbinguni Amenifurahisha
1. Baba yetu aliye mbinguni
amenifurahisha kwa kweli.
Kaniambia rohoni mwangu
Yesu yu nami, ananipenda.
Anipenda Yesu Mwokozi,
anipenda, anipenda.
Anipenda Yesu Mwokozi,
anipenda kweli.
2. Nimwachapo nikaenda mbali,
Yeye yu vivyo, ananipenda.
Akaniita kwake upesi,
Yesu yu nami, ananipenda.
Anipenda …
3. Anipenda, nami nampenda
wokovu wangu ulipokuja.
Tukimwona kufani Golgota,
Yesu yu nami, ananipenda.
Anipenda …
4. Kujua haya kwanipa raha,
kumtegemea kuna furaha.
Amfukuzapo hivi Shetani,
Yesu yu nami, ananipenda.
Anipenda …
5. Sifa ni nyingi asifiwazo,
moja ni kubwa katika hizo.
Hata mbinguni nitamwimbia
Yesu yu nami ananipenda!
Anipenda …
Comments
Post a Comment