312. Nakuapia Yesu
1. Nakuapia Yesu kukutumikia
Wewe u mfunzi wangu
na rafiki mwema.
Sitaogopa vita nikikufuata
siipotezi njia ukiniongoza.
2. Dunia i karibu, Bwana unilinde,
na majaribu mengi
yako pande zote.
Adui siku zote ni ndani na nje,
Ee Yesu univute karibu na Wewe!
3. Nazisikia sauti
zenye tamaa mbaya,
na mambo ya dunia
yanivuta sana.
Ee Bwana sema nami,
furaha iwe kuu,
nitakusikiliza,
Wewe mlinzi wangu.
4. Waagana na wote wakufuatao,
kwamba uliko Wewe,
nao watakuwa.
Nami ninaagana kukutumikia,
Yesu nisaidie kukuandamia.
5. Hatua zako Bwana
naziona wazi,
nizikanyage vema
hapa duniani.
Nishike hata mwisho,
Ee Yesu Mwokozi,
nichukue nikifa
na kwako mbinguni.
Comments
Post a Comment