250. Baba Uliye Mbinguni
1. Baba uliye mbinguni
tunakuomba kwa mioyo.
Twakuomba kama wana
waombavyo baba zao,
twaamini: Baba yetu
watusikia mbinguni.
2. Jina lako litakaswe
likitangazwa popote,
walisikiao Neno
walifuate kwa bidii.
Tulitumie vizuri
Jina la Mungu Mwenyezi.
3. Na ufalme wako uje
kwa mataifa mengine.
Tupe roho na rehema
tuzishike amri zako.
Ufalme wako ukae
katika mioyo yetu.
4. Utakayo yatimizwe
duniani kama mbinguni.
Shetani, mwili, dunia,
wasituzuie sisi,
kuyatenda mambo mema
na kukutii mpaka kufa.
5. Utupe leo chakula
chetu cha kututunzia,
tupate afya, chakula,
mavazi, mali, na jamaa,
serikali ya amani,
tutakushukuru Baba.
6. Tuondolee makosa
yasitusumbue tena,
tulivyowaondolea
na waliotukosea.
Tuwasaidie kama
unavyotusaidia.
7. Usituingize sisi
majaribuni popote.
Shetani asidanganye
na kutushinda kwa hila.
Ila tukijaribiwa
tushinde kwa nguvu zako.
8. Tuokoe maovuni
yoyote, Bwana, yalivyo,
ya mwili hata ya moyo
ya mali na ya heshima;
mwisho tutakapokufa,
tufe tukitengemana.
9. Kwani wako ni ufalme
nguvu nao utukufu
hata milele hakuna
vinavyokushinda wewe.
Kwa Jina la Mwana wako
kubali maombi yetu.
10. Ameni! Yatafanyika
yote tuliyokuomba.
Utaitika: Ameni,
tukikuomba kwa moyo.
Ameni ni kuambiwa:
“yatafanyika kwa kweli!”
Comments
Post a Comment