319. Yesu Unipendaye

1. Yesu unipendaye 

   kwako nakimbilia, 

   ni wewe utoshaye 

   mwovu akinijia; 

   yafiche ubavuni 

   mwako maisha yangu; 

   Nifikishe mbinguni, 

   wokoe moyo wangu.


2. Ngome nyingine sina,

   Nategemea kwako. 

   Usinitupe Bwana,

   nipe neema yako, 

   ninakuandamia 

   mwenye kuniwezesha; 

   Shari wanikingia,

   vitani wanitosha.


3. Nakutaka Mpaji 

   vyote napata kwako;

   Niwapo mhitaji, 

   utanijaza vyako;

   Nao waangukao

   wanyonge wape nguvu; 

   Poza wauguao.

   Uongoze vipofu.


4. Bwana umeniosha

   moyo kwa damu yako;

   Neema ya kutosha 

   yapatikana kwako; 

   Kwako Bwana naona, 

   kisima cha uzima:

   mwangu moyoni, Bwana, 

   bubujika daima.

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu