287. Mwamba Wangu wa Kale
1. Mwamba wangu wa kale,
kwako nitajificha.
Maji na damu yako
toka mbavuni mwako
ziwe dawa ya dhambi,
kutakasa mioyo.
2. Si kazi ya mikono
iletayo wokovu.
Nikitoa machozi,
nikifanya na bidii
siwezi kujiosha,
unioshe wewe tu.
3. Mkononi sina kitu,
ila msalaba wako,
ni mtupu, nipe nguo;
ni mnyonge, nipe nguvu;
niondolee taka,
nitakase sijafa.
4. Nikaapo duniani,
nifikapo kifoni,
nitakapofufuka,
nitakapokuona;
Mwamba wangu wa kale,
kwako nitajificha!
Comments
Post a Comment