266. Pote Atawala Nani?

 

1. K: Pote atawala nani? 

W: Pote atawala nani? 

K: Ni nani? 

W: Ndiye Mungu Mwenyezi.


2. K: Msifuni Mungu wetu, 

W: Msifuni Mungu wetu 

K: Yu Bwana, 

W: Vyote ni mali yake.


3. K: Mwumba jua nao mwezi, 

W: Mwumba jua nao mwezi? 

K: Na nyota 

W: Kwani anayo enzi.


4. K: Sasa wewe roho yangu, 

W: Sasa wewe roho yangu 

K: Kubali, 

W: Nyenyekea kwa Mungu.


5. K: Roho isiyotulia, 

W: Roho isiyotulia, 

K: Na Bwana, 

W: Haitapata raha.


6. K: Amemtuma Mwana wake, 

W: Amemtuma Mwana wake,

 K: Yesu Kristo, 

W: Ili atuokoe.


7. K: Amemshinda shetani, 

W: Amemshinda Shetani,

 K: Na dhambi, 

W: Na kutupa uzima.


8. K: Asimamisha agano 

W: Asimamisha agano, 

K: La Bwana,

W: Haleluya, ee Yesu.


9. K: Dunia wamsifu, 

W: Dunia wamsifu

 K: Kwa shangwe, 

W: Kwa kuwa hututunza.


10. K: Watawala na raia, 

W: Watawala na raia, 

K: Na waje, 

W: Wamshukuru Mwokozi.


11. K: Tumsifu Mungu Baba, 

W: Tumsifu Mungu Baba, 

K: Na Mwana 

W: Na Roho Mtakatifu.


12. K: Yatupasa kushukuru,

 W: Yatupasa kushukuru

 K: Upendo, 

W: Ulio wa milele.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu