313. Kwa Neema na Pendo

1. Kwa neema na pendo 

   ameniweka huru,

   si ustahili wangu,

   si haki na matendo. 

       /: Ni Yesu, Bwana 

        wangu, 

        Kwa neema ’meniweka 

        huru./:


2. Kwa moyo wa ubaba

   ameniweka huru,

   si kwa sababu zangu,

   si kwa ujuzi wangu. 

           Ni Yesu, …


3. Kwa utakaso wake 

   amesamehe yote; 

   Amefuta madeni 

   na dhambi na ujinga.

           Ni Yesu, … 


4. Kwa damu ya thamani 

   amelipia yote;

   Na vyeti vya madai 

   amepasua vyote, 

          Ni Yesu …


5. Kwa ukubali wake 

   amekubali wote: 

   Wenye mizigo wote 

   huwapumzisha vema. 

         Ni Yesu, …


6. Ijapo dhambi zenu 

   nyekundu kama damu;

   Kwa damu takatifu

   na iwe kama pamba. 

         Ni Yesu, …


7. Kwa neema na pendo 

   amejitoa kwangu!

   Mimi na nyumba yangu 

   tunajitoa kwake. 

         Ni Yesu, … 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu