288. Masikini Bartimayo

1.  Masikini Bartimayo 

    alikaa njiani, 

    alikuwa  akiomba 

    haja za kimwili.

 

2.  Akasikia sauti kuu 

    ya jeshi la watu, 

    akauliza upesi:  

    Kuna nini ndugu?

 

3.  Ndiye Yesu Mnazareti, 

    anapita sasa.

    Papo hapo Bartimayo 

    akaita sana.

 

4.  Ee Yesu, mwana Daudi,

    mimi nakuomba, 

    sasa unihurumie

    kipofu, masikini!


5.  Bwana Yesu kwa huruma

    akamwita aje.  Sema:

    Watakani kwangu?  

    Nikufanyieje? 


6.  Mimi Bwana ni kipofu, 

    nataka nione,

    nakuomba sana Bwana 

    unihurumie! 


7.  Na Yesu akamwambia: 

    Nenda zako sasa. 

    Imani inakuponya! 

    Mara akaona. 


8.  Sote tu vipofu Bwana 

    utuhurumie!

    Macho yetu yafumbue,

    Na tukufuate!


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu