285. Nilikuwa Kondoo
1. Mimi ni mtu mkosaji,
ni mwenye moyo mnyonge,
mwenye uchafu mwingi.
Mungu nihurumie!
2. Wema sina kabisa,
lakini maovu tu,
nimepunguka sana.
Mungu nihurumie!
3. Moyo umevunjika,
nina woga kwa macho
kutazama mbinguni.
Mungu nihurumie!
4. Yuko mmoja mbinguni,
ndiye mwokozi wetu,
nami ninamngojea.
Mungu nihurumie!
5. Niliyemtegemea,
Yeye hatanitupa,
anipenda kwa moyo.
Mungu nihurumie!
Comments
Post a Comment