284. Ninakulilia Mungu

1.  Ninakulilia Mungu 

    katika shida kubwa. 

    Usikilize maombi

    na sala kwa rehema. 

    Kwani ukiyahesabu 

    makosa yetu na dhambi,

    aponaye ni nani?


2.  Inatupasa rehema 

    tuondoshwe mabaya.

    Kutenda kwetu ni bure,

    tujapofanya mema. 

    Hakuna anayeweza  

    kujisifu mbele yako,

    wataka tu huruma.


3.  Sababu hii inanifaa

    kumtumaini Mungu; 

    rehema yake ni kubwa

    aliyoniwekea.

    Nashika Neno lake tu 

    lenye tulizo kubwa mno;

    Mungu ana rehema.


4.  Nikiwa na shida nyingi 

    sababu ya makosa.

    Sishindwi nazo, siachi 

    kumtumaini Mungu.

    Wakristo wa kweli wote 

    wanafuata njia hii, 

    kungoja saa ya Mungu.


5.  Dhambi zetu nyingi sana 

    hazishindi rehema.

    Mungu ni mweye nguvu kuu

    za kuzifuta zote. 

    Mchungaji mwema ni yeye

    atakayetuokoa tutoke

    makosani.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu