253. Nakuimbia Wewe Bwana

1. Nakuimbia wewe Bwana 

   hakuna mwingine kama wewe.

   Nakuimbia nyimbo zangu, 

   unipe nguvu ya roho wako,

   anifundishe nyimbo za sifa,

   niziimbe kwa Jina la Yesu.


2. Baba nivute kwa Mwanao,

   Mwanao anivute na kwako.

   Mtakatifu uniongoze,

   mawazo yangu yawe mazuri.

   Amani yako ikae mwangu,

   nikuimbie kwa furaha kuu.


3. Ukinisaidia hivi,

   Bwanangu nitaweza kuimba

   kukusifu wewe vizuri

   kwa roho na kwa kweli kila saa.

   Maana Roho anaongoza 

   niimbe malaika waimbavyo.


4.  Naomba nilivyofundishwa  

    na Roho wako yakupendeze.

    Nawe unasikia yote 

    sababu ya Mwana wako Yesu,

    aliyenifanya mtoto wako

    na mrithi wa ufalme wa mbingu.


5.  Ni heri nikijua haya!

    Naweza kukuomba vizuri:

    Najua kila kitu chema 

    nitakachoomba nitapewa,

    sababu kila kipaji chema

    kinashuka kutoka kwa Baba.


6.  Naomba kwa Jina la Yesu

    aniombeaye kwake Mungu. 

    Lolote nitakaloomba 

    kwa Jina lake Bwana anipa. 

    Sababu hii nakusifu Bwana,

    nakushukuru kwa nyimbo zangu. 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu