272. Twakuomba, ee Baba Mungu

K:  Twakuomba, Ee Baba Mungu,

    tupe rehema ya kimbingu;

    Tuwe watu wa Mungu.

W:  Wa utukufu.


1.  W:  Baba yetu uliye mbinguni, 

        Jina lako tutalitukuza,

        mapenzi yako ni ya makini 

        mbinguni na duniani.


2.  K:  Tupe leo riziki yetu,

        tusamehe makosa yetu 

        kama sisi tunavyosamehe  

        wanaotukosea.

  

3.  W:  Usitutie majaribuni, 

        Tuokoe na yule mwovu, 

        kwani wako ndio ufalme 

        sasa na hata milele. 

K:  /: Utukufu ni wako 

W:  Hata milele: 

K:  Utukufu ni wako 

W:  Hata milele. 

K:  Utukufu ni wako 

W:  Hata milele.

K:  Utukufu milele  Amen:/

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu