303. Neno Moja Bora Sana
1. Neno moja bora sana,
lishindalo mengine.
Mambo yote ya dunia
ndiyo mzigo mzito tu,
unaotutesa miili na roho,
lakini hayatunyang’anyi furaha.
Nikiwa na moja lililo bora
naona furaha isiyoisha.
2. Roho ukitaka hili,
hulioni kwa watu.
Acha mambo ya dunia,
hima nenda mbinguni,
alipo Mwokozi
pamoja na Mungu,
palipo na nguvu
na haki na kweli,
ndipo utakapoliona lile
linalokupasa hapa na huko.
3. Kumbuka Maria pale
miguuni pa Yesu.
Alivyosikia Neno alilohubiriwa.
Hakuna jingine alilolipenda
kuliko maneno ya
Yesu Mwokozi;
hakuna mawazo aliyowaza
kuliko kumwona na kumsikia.
4. Hivyo hata moyo wangu
unamtaka Yesu tu.
Unisaidie Bwana,
nikushike daima.
Naona wengine wapenda dunia,
na mimi napenda tu kukufuata.
Neno lako Yesu lenye uzima,
lanipa furaha isiyoisha.
5. Moyo wangu unaona
raha na amani tu.
Kwani Yesu Mchunga
wangu anilisha vizuri.
Sijui furaha ipitayo hii
ya kuwa na Yesu
na kumtumikia.
Sijui yawezayo kunitosha
kuliko kumshika
kwa nguvu zote.
6. Yesu wewe peke yako
u hazina yangu kuu.
Utazame moyo wangu,
unafiki ung’oe.
Nionye, nikiwa katika hatari
ukaniongoze nipate uzima.
Nijue: Dunia ni taka tupu,
kumjua Mwokozi ni neno bora.
Comments
Post a Comment