317. Cha Kutumaini Sina
1. Cha kutumaini sina
ila damu yake Bwana,
sina wema wa kutosha
dhambi zangu kuziosha;
Kwake Yesu nasimama,
ndiye Mwamba ni salama
ndiye Mwamba ni salama.
2. Njia yangu iwe ndefu
Yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga
nguvu zake ndiyo nanga.
Kwake Yesu …
3. Damu yake na sadaka
nategemea daima,
yote chini yakiisha
Mwokozi atanitosha.
Kwake Yesu …
4. Nikiitwa hukumuni,
rohoni nina amani;
Nikivikwa haki yake
sina hofu mbele zake.
Kwake Yesu …
Comments
Post a Comment