290. Wakosaji Fikirini

1.  Wakosaji fikirini 

    mwisho wa njia zenu! 

    Hamwogopi kupotezwa 

    vibaya kuzimuni? 

         Rudini kwake Mwokozi! 

         Ndiye mwenye huruma, 

         hawatupi wamjiao,   

         njooni tu kwake Yesu!


2.  Hapo mlipoyafuata

    mambo ya dunia hii,

    hamkuweza kuvivunja 

    vifungo vya Shetani.

         Rudini kwake …


3.  Mambo yote hugeuka, 

    tukimjua Mwokozi;

    twaondolewa makosa, 

    tuwe wake Bwana tu.

           Rudini kwake …


4.  Wote wampendao Bwana

    huwagawia mema;

    njooni nanyi myapokee 

    hayo mema ya mbingu! 

           Rudini kwake …


5.  Mpokeeni mioyoni 

    hamwezi kujilinda! 

    Lakini akiwatia 

    nguvu zake mwapona.

           Rudini kwake …


6.  Njooni na kumwangukia,

    awaokoe nanyi! 

    Atawapokea vema,

    msifuni siku zote. 

          Rudini kwake … 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu