305. Unishike! Mimi ni Mnyonge

1. Unishike!

   Mimi ni mnyonge sana 

   siwezi kwenda pasipo Wewe.

   Unishike! 

   Uliye Mponya wangu, 

   hofu na taabu hainishindi.


2. Unishike! Ukanivute kwako,

   niwe karibu na moyo wako.

   Unishike! Kwani nakosa njia

   nzuri nikienda peke yangu.


3. Unishike! Naona giza tupu 

   nisipouona uso wako.

   Lakini nuru yako iking’aza 

   njia yangu naona furaha.


4. Unishike! Utakaponiita niende

   kulazwa kaburini.

   Mwanga wako utokao 

   mbinguni

   uning’azie njia ya mwisho.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu