314. Ni Mpweke Hivi
1. Ni mpweke hivi sina rafiki.
Mwenzangu Yesu,
Yeye yu nami.
Ananifariji katika njia,
Ananifariji katika njia.
2. Wenzangu wote, wanichukie,
wakiniacha sitaogopa.
Pendo lake Yesu
ni ngome yangu,
pendo lake Yesu
ni ngome yangu.
3. Kazini mwangu dhiki napata.
Ingawa hivyo Yesu simwachi.
Ananiongoza na kuhifadhi,
Ananiongoza na kuhifadhi.
4. Ee moyo wangu usiogope.
Jikaze sasa, Yesu Mwenzio.
Atakuokoa katika shida,
Atakuokoa katika shida.
Comments
Post a Comment