300. Mimi ni Mwana Kondoo


1. Mimi ni Mwana Kondoo 

kikundini mwa Yesu, 

ninafurahishwa sana

 na Mchungaji wangu

 mwema; anipenda kabisa,

 anilisha vizuri.


2. Yeye akinilisha, 

ninatunzwa vizuri 

sina njaa, wala kiu, 

sina shida, wala hofu, 

ninaona raha tu 

na furaha moyoni.


3. Heri yangu ni kubwa 

nipendwaye na Yesu, 

siku zangu zikiisha, 

anipeleka mbinguni 

anikumbatiapo 

Yesu Mchungaji mwema.

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu