256. Njooni Tumsifu Mungu

1.  Njooni tumsifuni Mungu 

    aliye Mwenyezi,

    Mfalme wa popote 

    mbinguni na duniani.

    Kwa sauti kuu

    wote wamsifu Mungu, 

    kumpigia Mfalme shangwe.


2.  Njooni tumsifuni Mungu

    anayetawala, 

    vyote vizuri 

    akuongozaye na wewe.

    Waruka juu

    kama kwa nguvu ya tai,

    ukiongozwa na Mungu.


3.  Njooni tumsifuni Mungu

    aliyetuumba

    aliyetupa uzima

    na wingi wa neema. 

    Shida nyingi 

    zimefukuzwa kwetu,

    na Mungu mwenye rehema.


4.  Njooni tumsifuni Mungu 

    aliyetulinda,

    atubariki kwa pendo, 

    atupa riziki.

    Ni Mwenyezi,

    atutendea makuu,

    anatupenda kwa kweli.


5.  Njooni tumsifuni Mungu,

    tumsifu kwa nyimbo,

    kama Daudi imbeni 

    na mashangilio. 

    Tusisahau ndiye nuru ya roho.

    Tumsifu hata milele. 


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu