268. Msingi wa Kanisa
1. Msingi wa Kanisa
ndiye Yesu Bwana;
kiumbe kipya chake,
alipenda sana; kutaka litafuta
alishuka chini, naye kwa kuja
kwake akafa mtini.
2. Lina kila taifa, kisha ndilo moja,
wokovu wake una
Mwokozi mmoja;
Uzazi ni mmoja, na moja imani,
chakula ni kimoja, moja tumaini.
3. Watu hustaajabu
kwa mashaka mengi
yawapatayo nje hata ndani pia.
Ila watakatifu huomba,
wakesha usiku ni kilio,
asubuhi raha.
4. Mashaka na taabu
hata vita vyake,
vyangoja matimizo
ya amani yake,
ndipo kwa macho yetu
tuone utukufu
Kanisa lishindalo litastarehe juu.
Comments
Post a Comment