316. Ati Tuonane Mtoni?

1. Ati tuonane mtoni?

   Maji mazuri ya mbingu;

   Yanatokea mwangani, 

   penye kiti cha Mungu.

         Naam, tuonane mtoni!

         Watakatifu, 

         kwenu ni mtoni! 

         Tutakutanika mtoni 

         penye kiti cha Mungu.


2. Tukitembea mtoni 

   na Yesu Mchunga wetu 

   daima tu ibadani

   usoni pake kwetu.

         Naam, tuonane …


3. Kwang’ara sana mtoni,

   cha Mwokozi ni kioo, 

   milele hatuachani 

   tumsifu kwa nyimbo. 

         Naam, tuonane …


4. Si mbali sana mtoni 

   karibu tutawasili,

   mara huwa furahani 

   na amani ya kweli.

          Naam, tuonane … 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu