251. Moyo Wangu Furahiwa
1. Moyo wangu furahiwa,
tazama neema ya Bwana
katika mwaka huu.
Tazama mashamba yote
yanavyostawi vizuri,
yakupendeza wewe,
yakupendeza wewe.
2. Miti yote yachipuka
Yote yatoa maua
yanayong’aa vizuri.
Milima hata mabonde
tena nyika zimepambwa
kupita nguo zote,
kupita nguo zote.
3. Chore alia hewani,
vichakani kurumbiza
porini ni kulungu.
Pote sauti za wanyama,
Muumbaji azisikia
sifa za hivi vyote,
sifa za hivi vyote.
4. Mwenyezi Mungu bariki
vyote ulivyoviweka
chini ya mbingu yako.
Na mioyo yetu ing’ae
kwa neema yako nzuri mno
uliyotupa wewe,
uliyotupa wewe.
Comments
Post a Comment