306. Yesu Hukaribisha

1. Yesu hukaribisha

   wenye mabaya! Pasheni 

   wote waliokosa

   Neno hili la faraja, 

   walisikie vema:

   “Yesu ndiye Mwokozi.”


2. Twastahili kufa tu,

   Yesu hutuhurumia, akatufungulia

   mlango wa rehema kubwa.

   Nasi sasa twajua:

   “Yesu ndiye Mwokozi.”


3. Akipotea kondoo,

   Mchunga mwema amtafuta.

   Yesu Mchunga wa watu

   anawatafuta wote 

   waliokosa njia:

  “Yesu ndiye Mwokozi.” 


4. Yesu hukaribisha

   wakosaji, hata mimi 

   ameniita kwake, 

   mbingu imefunguliwa. 

   Naungama nikifa: 

   “Yesu ndiye Mwokozi.”


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu