294. Mtumwa wa Yesu Huona

1.  Mtumwa wa Yesu huona

    furaha nyingi mno.

    Si mtumwa wa unyang’anyi,

    ni mtoto wa Mungu.


2.  Mtumwa wa dhambi  haoni 

    njia ya wokovu.

    Mtumwa wa Yesu hakosi 

    njia ya mbinguni.


3.  Mpenda makosa huona 

    ugomvi na shida.

    Watu wa Yesu huona 

    upendo na raha.


4.  Ubaya wapata kufa,

    ni mshahara wake. 

    Yesu atuokoaye 

    aleta uzima.


5.  Bwana, umenikomboa 

    nami nakupenda, 

    nakutumikia wewe 

    simtaki mwingine.


6.  Nakuomba Bwana Yesu,

    unipeleke juu;

    ulipo ndipo pazuri 

    pa mtumishi wako.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu