282. Mimi Mkosaji Nakuomba

1.  Mimi mkosaji nakuomba 

    Mungu wangu Mtakatifu: 

    Uniendee kwa upole,

    nisipotee kabisa.

    Uliye na huruma kuu,

    Mungu, unihurumie!


2.  Naona hofu kubwa sana 

    kwa ajili ya makosa. 

    Nisaidie kwa rehema, 

    niliye mwenye ubaya. 

    Uliye na huruma …


3.  Unisikie Baba yangu, 

    nikikulilia sasa.

    Yaondoe makosa yangu, 

    moyo upate kupoa.

    Uliye na huruma …


4.  Usinitupe kwa ukali 

    kama nilivyostahili. 

    Unikubali tena, Baba, 

    katika kundi la wana. 

    Uliye na huruma …


5.  Ni neno hili liwezalo 

    kunipa tena moyo mkuu; 

   “Makosa yameondolewa 

    Nawe usikose tena”

    Uliye na huruma …


6.  Najua umenisikia,

    sioni shaka moyoni. 

    Sababu hii ninamaliza 

    kuomba kwangu kwa moyo.

    Uliye na huruma …


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu