302. Mungu Wetu Ndiye Boma

1. Mungu wetu ndiye boma, 

   silaha tena ngao, 

   atukingiaye shida

   zitushikazo sisi.

   Adui wa kale

   afanya hila ya kutushinda,

   ni mwenye nguvu kuu, 

   hakuna amwezaye.

 

2. Nguvu zetu hazifai

   tunashindwa upesi.

   Lakini tunaye shujaa 

   aliye mwenye nguvu. 

   Jina lake nani?

   Ni Yesu Kristo

   Mungu mwenyewe,

   hapana mwingine

   ni mshindaji wa wote.


3. Shetani akikusanya 

   majeshi yake yote.

   Hatuogopi kabisa 

   kwani tutawashinda!

   Mfalme wa dunia akunja uso

   ana hasira, lakini ni bure:

   Neno moja tu lamweza! 


4. Neno la Mungu lashinda!

   Halitafuti msaada. 

   Mungu yu pamoja nasi na roho 

   ya hekima. Wakitunyang’anya 

   watoto wenzi;

   mwili na mali haidhuru!

   Si kitu!

   Twamshika Yesu Mfalme.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu