274. Ewe Bwana Ndiwe Mchunga

1.  Ewe Bwana ndiwe 

    Mchunga wangu mwema.

    Sitapungukiwa na kitu, 

    kwani u pamoja nami.


2.  Wanilaza kwenye 

    malisho tele; 

    Wanitangulia vizuri,

    kwani wanipenda sana.


3.  Nafsi yangu 

    imehuishwa nawe,

    na kuongozwa kwa haki,

    kwa ajili ya Jina lako.


4.  Nikipita hata 

    bonde la mauti, 

    sitayaogopa mabaya,

    kwani Wee u gongo langu.


5.  Umeandaa meza 

    mbele yangu mimi,

    ili na watesi waone, 

    kwamba ndiwe mwenye neema.


6.  Kichwa changu 

    kimepakwa na mafuta,

    Kombe langu linafurika; 

    Haya umefanya yote.


7.  Wema wako

    umenifuata hasa.

    Nami nitaishi na wewe,

    kwako, Bwana siku zote. 


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu