339. Ee Ndugu, Twendeni Kazini
1. Ee ndugu, twendeni
kazini kwa Bwana,
tufuate nyayo
za Bwana, mwenyewe;
kwa nguvu ya Roho
atiaye upya,
tupate upendo
wake wa ajabu.
Mfalme mkuu yuko juu
Ye shujaa siku hii
katika kazi hii
thawabu ni taji
atakapokuja mfalme.
2. Tukikesha sana,
tukimwomba Bwana
Yeye atatupa yale tuombayo.
Tuwe mashahidi:
“Aondoa dhambi,
aosha mioyo ya watu wajutao.”
Mfalme mkuu …
3. Tuwatafuteni watu wapotevu,
na tuwatulize watu wa huzuni
tuwatunze watu walio maskini:
tuwe nuru gizani, tuwaangaze.
Mfalme mkuu …
4. Tukimshambulia
yule mwovu mkubwa,
tumheshimu sana
Bwana Mungu wetu.
Kazi yetu ni hii!
Ee jamaa Twendeni!
Tukishinda, Bwana
atatupa tuzo.
Mfalme mkuu …
5. Tushangilieni
kwa nyimbo za shangwe,
tusifu uzuri ule wa mbinguni.
Siku ile Bwana akija atupa
taji la uzima, thawabu ya vita.
Mfalme mkuu …
Comments
Post a Comment