338. Mawimbi Yanavuma
1. Mawimbi yanavuma,
yachafuka sana.
Na wokovu hapana,
pwani hatuoni!
Giza liko popote,
Mmoja ndiye Mwokozi;
Bwana Yesu, tuokoe Bwana.
2. Mwezi ukichelewa,
nyota zikienda,
chombo kikivunjika,
Mwokozi ni nani?
Mwokozi ndiye Bwana,
Yeye nahodha wetu.
Bwana Yesu, tuokoe Bwana.
3. Mawimbi yatulia
kukiwa shwari kuu.
Wewe Muumbaji wetu
tunakushukuru;
twakuimbia Bwana,
leo na siku zote.
Bwana Yesu, tuokoe Bwana.
4. Shida za kufa kwangu
zinaponijia
Bwana uniokoe
nisizame mimi.
Unipe mkono wako
Wewe unipendaye.
Bwana Yesu, tuokoe Bwana.
Comments
Post a Comment