337. Wakristo Ifuateni

1.  Wakristo ifuateni 

    vita yake Mungu.

    Wote wachaguliwao 

    ondokeni hima. 

    Haya bendera juu 

    nyote fuateni! 

    Baragumu zinalia!

    Njooni, njooni nyote! 


2.  Askari wote waseme:

   “Mungu yuko kwetu.” 

    Mwokozi Yesu mwenyewe 

    atupigania. 

    Wote na malaika watusaidia.

    Pamoja na Shujaa wetu 

    twamshinda adui. 


3.  Kavumilieni taabu, 

    askari wa Yesu! Ikingieni mioyo

    mishale ya mwovu.

    Haya, yaacheni 

    mambo mapotovu. 

    Mfanya vita afikiri 

    mambo ya vita tu. 


4. Shikeni silaha zote 

   za vita kali hii.

   Upanga ulio mkali 

   ni Neno la Mungu.

   Lenu tegemeo liwe ngao yenu.

   Ukanda wa viunoni

   ni kweli na haki. 


5. Piganeni kwa kishujaa 

   kila siku vema. 

   Na Yesu awafundishe 

   mambo ya vita hii.

   Ngoja, watashinda 

   wao wenye bidii. 

   Taji yenu ni tayari; 

   Uzima wa mbingu. 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu