336. Tumfuate Bwana Yesu

1. Tumfuate Bwana Yesu,

   kiongozi ni Yeye; 

   atuonyeshaye njia 

   ya kushinda dunia. 

   Tukikaa ulimwenguni 

   twende njia ya mbingu,

   tupendane vizuri, 

   tuamini kwa mioyo.

   Yesu tutangulie 

   nasi twakufuata.


2. Tumfuate Bwana Yesu,

   hata tukiteseka.

   Hapa pana shida nyingi, 

   huko iko furaha. 

   Wapandao kwa machozi 

   watavuna kwa shangwe.

   Mungu atabadili

   kulia kuwe kucheka. 

   Tulipoteswa hapa 

   tutaona furaha.


3. Tumfuate Bwana Yesu,

   tufe pamoja naye.

   Kufa kwake kwatuponya 

   katika upotevu.

   Duniani tuishinde 

   miili yetu na tamaa;

   Yesu atufufua

   miili yetu kaburini. 

   Yesu nitakufia, 

   nikuone milele.


4. Tumfuate Bwana Yesu, 

   kwani amefufuka.

   Tena atawafufua 

   watu siku ya mwisho.

   Sisi tu viungo vyake,

   tutafika huko juu 

   enzini mwa mkuu wetu 

   aliyetuita kwake.

   Yesu nakupa moyo, 

   nipe uzima wako. 


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu