335. Sisi Tulio Watoto
1. Sisi tulio watoto
wa Mwenyezi milele.
Tupendane kama Yesu
alivyotufundisha.
Yote tunayotaka
watu watufanyie
na sisi tuwafanyie,
ndiyo amri ya Mwokozi.
2. Tutumikiane vema
kwa upendo wa nguvu.
Hivi tunazaa matunda
yampendezayo Mungu.
Tumsaidie ndugu
kwa hiari shidani,
tukumbuke hata sisi
twapewa vyote na Mungu.
3. Tusiwachukie ndugu
waliotukosea;
ila tupatane tena
tukisameheana.
Mwenye dhambi tumwonye
kwa upole na upendo:
hivi tutamsaidia,
asikose njia nzuri.
4. Tusiwahukumu ndugu
waliokosa sana.
Tukumbuke, hata sisi
tuna makosa mengi.
Tumsikie Mwokozi
akionya Wakristo;
Usimhukumu mwenzio,
ili usihukumiwe.
5. Bwana utuvike sote
mavazi ya uongofu.
Ututengeneze vema tule
karamu kwako
Mwisho uniambie;
Ewe mtumwa mwema
njoo ulikuwa mwaminifu,
nakupa furaha zangu.
Comments
Post a Comment