332. Njia Ile Nyembamba

1. Njia ile nyembamba 

   iendayo uzimani! 

   Heri anayekwenda

   njia hii na Bwana Yesu. 

   Kaza mwendo ufike, 

   usichoke njiani.


2. Heri waliokuwa 

   waaminifu hata kufa,

   walioshinda tamaa 

   wanaomfuata Yesu, 

   watapewa mshahara,

   taji ya washindao.


3. Yesu ametufia 

   msalabani kwa uchungu,

   akapaa mbinguni juu  

   akapata utukufu.

   Tutapewa uzima  

   tukimfuata Yesu.


4. Ndugu tusiogope 

   njia yenye shida nyingi.

   Kesheni muombeni 

   Bwana atutegemeze. 

   Tutaweza kushinda 

   tukimshika Yesu tu.


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu