331. Nivute Kwako Bwana Yesu

1.  Nivute kwako, Bwana Yesu,

    katika shida hata furaha, 

    unipokee kwa rehema, 

        /: niangalie,  

        ee Bwana wangu.:/


2.  Nivute kwako! Sina kitu 

    ninachoweza kukutolea,

    ila moyo huu wenye dhambi. 

        /: Yesu Mwokozi  

          unisafishe.:/


3.  Nivute kwako! Nitaacha 

    yote yazuiayo baraka. 

    Nakutolea, Bwana wangu. 

       /: mali na furaha  

         za dunia.:/


4.  Nivute kwako! Mpaka mwisho

    vita na hatari zikiisha. 

    Mpaka nifanane na Wewe, 

       /: Wewe, ee Yesu,  

          furaha yangu!:/ 


Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu